- Kidhibiti Maudhui: Zana ya wavuti kwa washirika wanaodhibiti maudhui na haki kwenye YouTube. Akaunti ya Kidhibiti Maudhui inamiliki kituo kimoja au zaidi cha YouTube na vipengee vinavyohusishwa nazo. Inajulikana pia kama Kidhibiti Maudhui cha Studio.
- Msimamizi: Mtu anayesimamia Kidhibiti Maudhui na kualika wengine kukifikia.
- Mtumiaji: Yeyote anayetumia Kidhibiti Maudhui.
Kuweka mipangilio ya Kidhibiti chako cha Maudhui
1. Unganisha chaneli zakoKidhibiti Maudhui kinaweza kuunganisha chaneli nyingi kwa kuanzisha chaneli au kualika chaneli nyingine zijiunge na akaunti ya Kidhibiti Maudhui.
Baada ya kuunganisha chaneli, unaweza kupakia maudhui kwenye chaneli hiyo, ili kudhibiti uchumaji wa mapato ya video zake na kuweka chapa kwenye chaneli hiyo.
Ili uchume mapato na kupokea malipo kutokana na video zako, unahitaji kuhusisha akaunti ya AdSense katika YouTube na akaunti yako ya Kidhibiti Maudhui. Unaweza kufungua akaunti ya AdSense katika YouTube au uhusishe akaunti iliyopo.
Kwenye ukurasa wa Mipangilio , unaweza kuteua machaguo ya upachikaji na kanuni za kubainisha ya Kidhibiti chako cha Maudhui.
Ili ubadilishe sarafu chaguomsingi, nenda kwenye Mipangilio Mapendeleo ya Mtumiaji kisha uchague sarafu ambayo ungependa kutumia. Mabadiliko haya hayaathiri sarafu ya malipo iliyobainishwa katika akaunti ya AdSense katika YouTube. Ukilipwa kwa sarafu hiyo, kiasi kinachoonyeshwa hapa bado huenda kikawa tofauti na pesa utakazopokea kutokana na viwango tofauti vya ubadilishaji sarafu.
Unaweza pia kuchagua hatua chaguomsingi kwa kampeni katika Mipangilio Kampeni. Kwa madai ya Content ID, unaweza kuchagua kuangazia video zako rasmi zinazopakiwa na mashabiki au kutofanya lolote. Kampeni maalum zinaweza kubatilisha mipangilio hii.
Unaweza kuwaalika watumiaji wengine wajiunge kwenye akaunti ya Kidhibiti Maudhui ili wadhibiti maudhui yake.
YouTube inapofungua akaunti ya Kidhibiti Maudhui, mtumiaji mmoja au zaidi huwa wasimamizi wa akaunti hiyo. Pamoja na kualika watumiaji, wasimamizi pia wanaweza kuanzisha majukumu ya mtumiaji ambayo hubainisha vipengele na vikwazo vinavyotumika kwa watumiaji tofauti.