Sera kuhusu usalama wa watoto

Usalama wa watayarishi, watazamaji na washirika wetu ndio kipaumbele chetu cha juu zaidi. Tunamtegemea kila mmoja wenu atusaidie kulinda jumuiya ya kipekee yenye hamasa ya hali ya juu. Ni muhimu kuelewa Mwongozo wetu wa Jumuiya pamoja na jukumu lake kwenye wajibu wetu wa pamoja wa kuifanya YouTube kuwa sehemu salama. Tenga muda usome kwa uangalifu sera iliyo hapa chini. Pia unaweza kutembelea ukurasa huu ili upate orodha kamili ya mwongozo wetu.
Taarifa: Haturuhusu maudhui yanayolenga watoto wadogo na familia, yaliyo na mada za ngono, vurugu, lugha chafu au mada nyingine za watu wazima ambazo hazifai hadhira za watoto kwenye YouTube. Mbali na mada, maelezo na lebo zako, hakikisha kuwa hadhira unayochagua inalingana na hadhira inayolengwa na maudhui yako.

YouTube hairuhusu maudhui ambayo yanahatarisha hali ya watoto kihisia na kimwili. Mtoto ni mtu aliye chini ya umri wa miaka 18.

Ikiwa utaona maudhui yanayokiuka sera hii, yaripoti. Iwapo unaamini kuwa mtoto yuko hatarini, unapaswa kuwasiliana na taasisi ya sheria katika eneo uliko ili uripoti hali hiyo mara moja.

Maagizo ya kuripoti ukiukaji wa Mwongozo wa Jumuiya yetu yanapatikana hapa. Ikiwa umepata maoni au video nyingi ambazo ungependa kuripoti, unaweza kuripoti chaneli.

Katika hali fulani, tunaweza kutoa ruhusa za kutofuata kanuni kwa maudhui yaliyo na muktadha wa kielimu, kihalisia, kisayansi au kisanaa, ikiwa ni pamoja na maudhui ambayo ni ya maslahi ya umma.

Jinsi sera hii inavyokuathiri

Iwapo unachapisha maudhui

Usichapishe maudhui kwenye YouTube iwapo yanalingana na maelezo yoyote yaliyo hapa chini.

  • Kuwachukulia watoto katika mitazamo ya ngono: Maudhui dhahiri ya ngono yanayoangazia watoto na maudhui yanayowanyanyasa watoto kingono yakiwemo ya uchi wa watoto yaliyochapishwa kwa kusudi la ucheshi. Tunaripoti maudhui yanayoonyesha unyanyasaji wa watoto kingono kwenye Kituo cha Kitaifa cha Watoto Waliopotea na Wanaonyanyaswa, ambacho hufanya kazi na taasisi za utekelezaji wa sheria kote duniani.
  • Vitendo hatari au vya kudhuru vinavyohusisha watoto: Maudhui yanayoonyesha mtoto akishiriki katika shughuli hatari au yanayowahimiza watoto kufanya shughuli hatari, hasa ikiwa mtu anayetazama anaweza kuiga kitendo hatari au ikiwa maudhui yanahimiza au kusifu kitendo hatari. Kamwe usiwaweke watoto kwenye hali hatarishi ambazo huenda zikasababisha majeraha, ikiwa ni pamoja na vitendo hatari, mashindano, michezo ya kuthubutu au mizaha. Vitendo hatari vinajumuisha lakini si tu, kitendo chochote katika aina zilizoorodheshwa kwenye mashindano Hatari Zaidi, kama vile hali ya kunyuma pumzi au kupigwa shoti ya umeme.
    • Mifano inajumuisha maudhui yanayoonyesha watoto:
      • Wakinywa pombe
      • Wakitumia vivukisho, sigara za kielektroniki, tumbaku au bangi
      • Wakitumia vibaya fataki
      • Wakitumia bunduki bila usimamizi
  • Wakisababisha au kuendeleza madhara ya kimwili, kingono au unyanyasaji wa kihisia au kutelekeza mtoto, pamoja na kuwafadhaisha watoto kihisia.
    • Maudhui yanayoonyesha dhuluma kimwili, kingono au kihisia kwa mtoto katika muktadha wa kielimu, kihalisia, kisayansi au kisanaa na yaliyotiwa ukungu huenda yakaruhusiwa kutofuata kanuni ya sera.
    • Maudhui yanayoweza kusababisha watazamaji au washiriki watoto wawe na mfadhaiko wa kihisia, ikiwa ni pamoja na:
      • Kuwaonyesha watoto maudhui ya watu wazima
      • Kuiga unyanyasaji kutoka kwa wazazi
      • Kuwashurutisha watoto
      • Vurugu
  • Maudhui ya familia yanayopotosha: Maudhui yanayolenga watoto wadogo na familia, lakini yana:
    • Maudhui ya ngono
    • Vurugu
    • Maudhui machafu au maudhui mengine ya watu wazima ambayo hayafai hadhira za watoto
    • Taratibu za matibabu
    • Kujijeruhi
    • Utumiaji wa wahusika wa filamu za kuogofya za watu wazima
    • Maudhui mengine yasiyofaa yaliyokusudiwa kushtua hadhira ya watoto
    • Maudhui yanayolenga watoto wadogo na familia yenye mada zisizofaa umri fulani katika muktadha wa kielimu, kihalisia, kisayansi au kisanaa huenda yakaruhusiwa kutofuata kanuni ya sera. Hii si ruhusa ya kulenga watoto wachanga na familia na mada za watu wazima zinazolenga kuogofya hadhira za watoto.
    • Katuni zinazofaa familia zinazolenga watoto wadogo na zina maudhui ya watu wazima au yasiyofaa umri fulani, kama vile vurugu, ngono, kifo, dawa za kulevya na mengineyo. Haturuhusu maudhui yaliyowekewa lebo kwamba yanawafaa watoto katika jina, maelezo, lebo au katika uteuzi wa hadhira ya video ikiwa yana mada zisizofaa umri fulani.
    • Hakikisha kuwa mada, maelezo na lebo zako zinalingana na hadhira unayolenga. Isitoshe, hakikisha kuwa hadhira unayochagua inawakilisha hadhira inayolengwa na maudhui yako kwa njia sahihi. Unaweza pia kuweka mipaka ya umri kwenye maudhui yako baada ya kupakia iwapo yanalenga hadhira za watu wazima.
  • Uchokozi wa mtandaoni, unyanyasaji na upekuzi na utangazaji wa taarifa binafsi za watoto: Maudhui ambayo:
    • Yana nia ya kufedhehesha, kudanganya au kumtukana mtoto
    • Yanafumbua taarifa binafsi za mtoto, kama vile anwani za barua pepe au namba za simu, bila kujali iwapo zimetumwa na wengine au mtoto mwenyewe.
    • Yana marejeleo ya kingono
    • Yanawahimiza wengine kuchokoza au kunyanyasa

Sera hii inatumika kwenye video, maelezo ya video, maoni, machapisho, mitiririko mubashara, orodha pamoja na kipengele au bidhaa nyingine yoyote ya YouTube. Kumbuka kuwa orodha hii si kamili.

Tafadhali kumbuka kuwa sera hizi pia zitatumika katika viungo vya nje kwenye maudhui yako. Hii inaweza kujumuisha URL unazoweza kubofya, kuwaelekeza watumiaji kwenye tovuti nyingine katika video kwa kutamka, pamoja na njia nyingine.

Maudhui yenye mipaka ya umri

Tunaweza kuweka mipaka ya umri kwenye maudhui yanayojumuisha hali yoyote kati ya zifuatazo.

  • Vitendo hatari au vya kuumiza ambavyo watu wazima au watoto wanaweza kuiga: Maudhui yaliyo na watu wazima wakishiriki katika shughuli hatari ambazo watu wazima au watoto wanaweza kuiga kwa urahisi.
  • Mada za watu wazima katika maudhui ya familia: Maudhui yanayolenga hadhira za watu wazima lakini yanaweza kumkanganya mtu kwa urahisi afikiri kuwa ni maudhui ya familia. Maudhui haya yanajumuisha katuni zilizo na mada za watu wazima kama vile vurugu, ngono au kifo. Kumbuka kuwa unaweza kuweka mipaka ya umri kwenye maudhui yako baada ya kuyapakia, iwapo yanalenga hadhira za watu wazima.
  • Lugha chafu: Lugha nyingine haifai kwa watazamaji wadogo. Maudhui yanayotumia lugha chafu ya kingono au lugha chafu zaidi yanaweza kusababisha kuwekewa mipaka ya umri.
Maudhui yanayoangazia watoto
Ili kulinda watoto kwenye YouTube, tunaweza kuzima baadhi ya vipengele katika kiwango cha maudhui na chaneli kwenye maudhui yasiyokiuka sera zetu lakini yanaonyesha watoto au yamepakiwa na watoto. Vipengele hivi vinaweza kujumuisha:
  • Maoni
  • Gumzo la moja kwa moja
  • Kutiririsha mubashara
  • Mapendekezo ya video (jinsi na wakati ambao video yako hupendekezwa)
  • Machapisho
  • Kuandaa mseto wa Video Fupi
Kumbuka:
  • Tunaweza pia kutumia masharti makali zaidi kwenye uonyeshaji wa maoni, machapisho na ujumbe wa gumzo la moja kwa moja kwenye chaneli zinazomilikiwa na watoto au zinazohusiana na maudhui yanayoonyesha au yaliyopakiwa na watoto.
  • Mitiririko mubashara iliyo na watoto walio na umri wa chini ya miaka 16 ambao hawaonekani wakiwa na mtu mzima inaweza kuondolewa au magumzo ya moja kwa moja kuzimwa. Chaneli ambazo hazitii sera hii zinaweza kupoteza kwa muda au kabisa uwezo wa kutiririsha mubashara au idhini ya kufikia vipengele vingine.

Jinsi ya kuwalinda watoto katika maudhui yako

Kabla ya kuchapisha maudhui yanayokuhusu wewe, familia au marafiki zako, tafakari kwa makini iwapo yanaweza kuweka mtu yeyote katika hatari ya kuangaziwa kwa njia isiyofaa. Watoto ni watu walio katika hatari na YouTube ina sera za kuwalinda dhidi ya kuangaziwa kwa namna isiyofaa.

  • Hakikisha kuwa mtoto anasimamiwa na mtu mzima na anafanya shughuli zinazoambatana na umri wake kama vile kuonyesha mambo anayopenda, maudhui ya kielimu au maonyesho ya umma.
  • Hakikisha kuwa mavazi yanayovaliwa yanaambatana na umri. Jiepushe na mavazi ambayo hayamfuniki mtoto vizuri au yanayobana kabisa.
  • Tumia mipangilio ya faragha ya YouTube kudhibiti watu wanaoweza kutazama video unazochapisha.

Usichapishe kwenye YouTube maudhui yanayowaangazia watoto na yanayojumuisha hali moja au zaidi kati ya zifuatazo:

  • Yamerekodiwa katika maeneo ya faragha nyumbani kama vile vyumba vya kulala au mabafu.
  • Yanayoangazia watoto wakiomba anwani kutoka kwa watu wasiowajua, michezo ya kuthubutu au mashindano mtandaoni, au kujadili mada za watu wazima.
  • Yanaonyesha shughuli zinazoweza kuwavutia watoto kwa njia isiyotakikana, kama vile kufanya miondoko hatari ya mwili au msisimko (ASMR).
  • Yanafumbua taarifa binafsi kuhusu mtoto.

Hii ni baadhi tu ya mifano, unaweza kupata mbinu bora kuhusu usalama wa watoto hapa. Iwapo una umri wa chini ya miaka 18 au umri wa mtu mzima katika nchi uliko, Kutumia intaneti kwa uungwana kunaweza kukusaidia kuwa salama mtandaoni.

Mifano

Ifuatayo ni baadhi ya mifano ya maudhui ambayo hayaruhusiwi kwenye YouTube.

  • Video au machapisho yanayoangazia watoto wanaohusika katika vitendo vya kuthubutu, mashindano na shughuli za kuchochea ngono au mahaba, kama vile kupiga busu au kupapasana.
  • Maudhui yanayoonyesha watoto wakihusika katika shughuli hatari. Kwa mfano, matendo ya kustaajabisha, kwa kutumia silaha au vilipuzi au kutumia dawa zinazodhibitiwa kama vile pombe au nikotini ikijumuisha vivukisho au sigara za kielektroniki.
  • Video yenye lebo kama vile "inalenga watoto" au ambayo hadhira yake imewekwa kuwa “Ndiyo, inalenga watoto”, inayoangazia katuni zinazofaa familia zikihusika katika vitendo visivyofaa kama vile kuchoma sindano.

Kumbuka kuwa hii ni baadhi tu ya mifano na usichapishe maudhui iwapo unaona kuwa yanaweza kukiuka sera hii.

Mifano zaidi

  • Kutoa pesa, sifa, alama ya kupenda au motisha yoyote nyingine kwa mtoto ili ashiriki katika matendo ya kugusana na mtu mwingine.
  • Video au chapisho linalotangaza maudhui ya ngono yanayoangazia watoto au maudhui mabaya yanayoangazia watoto.
  • Tabia ya kunyatia inayohusisha mawasiliano na watoto au kuhusu watoto.
  • Kujumlisha maudhui mazuri ya watoto kwa madhumuni ya kuchochea ngono.
  • Maudhui ya ugomvi au uchokozi yanayoangazia watoto bila muktadha wa kielimu, kihalisia, kisayansi au kisanaa au kutiwa ukungu.
  • Mashindano, mizaha au matendo ya kustaajabisha yanayoweza kusababisha hatari ya majeraha ya mwili au mfadhaiko mkuu. Unaweza kupata maelezo zaidi kuhusu kisichoruhusiwa katika sera zetu kuhusu mashindano na mizaha.
  • Kuwahimiza watoto washiriki katika shughuli hatari, hata kama hakuna watoto katika maudhui hayo.
  • Maudhui yanayoiga unyanyasaji kutoka kwa wazazi au utelekezaji, kuiga matendo ya kukaribia kifo au vurugu, au kusababisha watoto kuwa na aibu kubwa au kudhalilishwa.
  • Kutumia katuni, vikaragosi au wahusika wa burudani ya familia ili kuwavutia watoto kwenye maeneo ambako maudhui yanaangazia mada za watu wazima kama vile vurugu na ngono.

Kitakachofanyika iwapo maudhui yanakiuka sera hii

Iwapo maudhui yako yanakiuka sera hii, tutaondoa maudhui hayo na kukutumia barua pepe ili kukufahamisha. Tukishindwa kuthibitisha kuwa kiungo ulichochapisha ni salama, huenda tukakiondoa. Kumbuka kuwa URL zinazokiuka sera zinazochapishwa kwenye video husika au katika metadata ya video zinaweza kusababisha tuondoe video hiyo.

Ikiwa hii ni mara yako ya kwanza kukiuka Mwongozo wa Jumuiya yetu, huenda ukapewa tahadhari bila adhabu kwenye chaneli yako. Utakuwa na chaguo la kushiriki katika mafunzo ya sera ili kuruhusu muda wa tahadhari uliopewa uishe baada ya siku 90. Kipindi cha siku 90 kitaanza baada ya mafunzo kukamilika, wala si wakati onyo limetolewa. Hata hivyo, ikiwa utakiuka sera hiyo tena ndani ya kipindi hicho cha siku 90, huenda muda wa tahadhari usiishe na chaneli yako inaweza kupewa onyo. Ukikiuka sera tofauti baada ya kukamilisha mafunzo, utapewa tahadhari nyingine.

Huenda chaneli yako ikasimamishwa ukipata maonyo 3 ndani ya siku 90. Pata maelezo zaidi kuhusu mfumo wetu wa maonyo.

Tunaweza kusimamisha chaneli au akaunti yako kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa Mwongozo wa Jumuiya au Sheria na Masharti. Tunaweza pia kusimamisha chaneli au akaunti yako baada ya tukio moja la ukiukaji kwa kiasi kikubwa au chaneli ikikiuka sera mara kwa mara. Huenda tukazuia watu wanaorudia kufanya makosa wasishiriki katika mafunzo ya sera siku zijazo. Pata maelezo zaidi kuhusu kusimamishwa kwa chaneli au akaunti.

YouTube hairuhusu kabisa maudhui ya unyanyasaji kwa watoto. Iwapo tunafikiri kuwa mtoto yuko hatarini kulingana na maudhui yaliyoripotiwa, tutawasaidia watekelezaji wa sheria wachunguze maudhui hayo.

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Programu za Google
Menyu kuu
12092231398829982089
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
false
true
true
true
true
true
59
false
false
false
false