Ili uthibitishe kituo chako, utaombwa uweke nambari ya simu. Tutatuma nambari ya kuthibitisha kupitia ujumbe wa maandishi au kupiga simu ya sauti kwenye nambari hiyo ya simu.
Baada ya kuthibitisha akaunti yako, unaweza:
- Kupakia video zenye urefu wa zaidi ya dakika 15.
- Kuweka vijipicha maalum.
- Kutiririsha mubashara.
- Kukata rufaa dhidi ya madai ya Content ID.
Huenda pia ukaombwa uthibitishe akaunti yako unapojisajili. Kumbuka: Si watoa huduma wote wanaruhusu ujumbe wa maandishi na/au simu za sauti kutoka Google.
Kwa nini YouTube inaomba nambari yangu ya simu?
Tunadhibiti taka na matumizi mabaya kwa umakini mkubwa. Kutumia nambari za simu kuthibitisha utambulisho ni njia moja ya kulinda jumuiya yetu na kukabiliana na matumizi mabaya.
Tunatumia nambari ya simu kukutumia nambari ya kuthibitisha. Pia, tunahakikisha kuwa nambari ya simu imeunganishwa kwenye vituo visivyozidi 2 kwa mwaka.
Sijapokea nambari ya kuthibitisha
Unatakiwa kupokea nambari ya kuthibitisha papo hapo. Ikiwa hujapokea, unaweza kuomba utumiwe msimbo mpya. Usipopokea msimbo, unaweza kuwa unakabiliwa na mojawapo ya matatizo haya ya kawaida:
- Baadhi ya watoa huduma hawaruhusu ujumbe wa maandishi au simu za sauti kutoka Google: Watoa huduma wengi wa simu wanaruhusu ujumbe wa maandishi kutoka Google. Unaweza kujaribu chaguo la ujumbe wa maandishi au simu ya sauti au utumie namba ya simu kutoka kwa mtoa huduma tofauti. Usipopokea msimbo mpya, kuna uwezekano kuwa mtoa huduma wako haruhusu ujumbe wa maandishi au sauti kutoka Google.
- Kuna akaunti nyingi zinazotumia namba sawa ya simu: Ukipata ujumbe kuhusu hitilafu unaosema, "Namba hii ya simu imeshafungua idadi ya juu zaidi ya akaunti inayoruhusiwa," itabidi utumie namba tofauti ya simu. Ili kusaidia kuzuia matumizi mabaya, namba ya simu inaweza tu kuunganishwa na chaneli 2 kwa mwaka.
- Ujumbe wa maandishi unaweza kuchelewa kufika: Ucheleweshaji unaweza kutokea katika maeneo yaliyo na watu wengi au ikiwa miundombinu ya mtoa huduma wako si thabiti. Ikiwa umesubiri kwa zaidi ya dakika kadhaa na bado hujapokea ujumbe wa maandishi kutoka kwetu, jaribu chaguo la kupigiwa simu ya sauti.