Huduma za Google Play ni programu msingi ya mfumo inayowezesha utendakazi muhimu kwenye kila kifaa cha Android kilichoidhinishwa. Kuna aina tatu za vipengele msingi vya kifaa ambazo zinatolewa na huduma za Google Play:
Usalama na uhakika
Huduma za Google Play zinasaidia kuhakikisha usalama na uhakika wa kifaa cha Android na kusasisha vifaa kwa kutumia vipengele vipya kabisa vya usalama. Hii ni pamoja na:
- Google Play Protect, ambayo inaweza kuwaonya watumiaji iwapo programu fulani ina programu hasidi inayojulikana.
- Kutambua na kuthibitisha miunganisho salama, kama vile kuruhusu kifaa kutambua na kuunganisha kiotomatiki na kwa usalama kwenye vifaa vingine au kutuma faili au programu kwenye vifaa vya Android vilivyo karibu.
- Kulinda programu dhidi ya ulaghai na vitisho vya usalama kupitia SafetyNet.
- Kuhifadhi nakala yako kupitia usimbaji fiche wa mwanzo hadi mwisho iwapo watumiaji wana namba ya siri ya skrini iliyofungwa.
- Kudhibiti na kulinda manenosiri yako.
API za Wasanidi Programu
Huduma za Google Play huwapa wasanidi programu maelfu ya API zinazosasishwa kila mara zinazowawezesha kuwasilisha hali ya utumiaji ya ubora wa juu katika programu zao, kama vile:
- Kutiririsha maudhui kupitia Google Cast.
- Kuunganisha Ramani za Google ili kuboresha utendaji wa programu.
- Kutoa maelezo sahihi ya mahali kupitia kwa mtoa huduma wa mahali palipokokotolewa iwapo programu zina ruhusa ya kupafikia.
- Kuwezesha huduma zinazoruhusu wasanidi programu kutayarisha miundo ya utangazaji kulingana na mipangilio ya programu na mtumiaji.
- Kutuma arifa kwa wakati ufaao kupitia safu ya uchukuzi ya ujumbe.
Huduma msingi za kifaa
Huduma za Google Play huwezesha huduma msingi kwenye vifaa vya Android. Kwa mfano:
- Watumiaji wanapopiga simu ya dharura kwa namba ya dharura inayotumika, Google husaidia huduma za dharura za karibu kupokea moja kwa moja data ya mahali kifaa kilipo.
- Huduma za kujaza kiotomatiki za Google huwasaidia watumiaji kuokoa muda na kupunguza hitilafu za kuandika.
- Kipengele cha Uhamishaji wa Karibu kinaruhusu watumiaji kutuma faili kwa anwani zao au kwa kuficha utambulisho wa data.
- Kipengele cha Tafuta Kifaa Changu hufanya iwe rahisi kutafuta, kufunga au kuondoa kifaa kilichopotea.
- Kipengele cha Kuunganisha Haraka hufanya iwe rahisi kuunganisha vifaa vya Bluetooth kwa kutumia akaunti yako ya Google.
Pia, mtumiaji anapoingia katika akaunti ya Google kwenye kifaa chake, anaweza kusasisha mipangilio yake kwenye Google, kudhibiti usalama wa akaunti yake na kusawazisha data muhimu, kama vile Anwani zake za Google, kwenye vifaa mbalimbali.
Kwa nini huduma za Google Play hukusanya data
Huduma za Google Play hukusanya data kwenye vifaa vya Android vilivyoidhinishwa ili kusaidia vipengele msingi vya kifaa. Ukusanyaji wa maelezo mahususi ya msingi, kama vile anwani ya IP, ni muhimu ili kuwasilisha maudhui kwenye kifaa, programu au kivinjari. Watengenezaji wa vifaa pia hutoa ruhusa kwa huduma za Google Play zifikie data fulani kwenye kifaa, kama vile mahali na anwani, ili kusaidia vipengele hivi.
Ukusanyaji data halisi hutofautiana kulingana na mipangilio kwenye kifaa iliyowekwa na mtumiaji, programu na huduma zilizowekwa au zinazotumika kwenye kifaa, mtengenezaji wa kifaa na mipangilio ya akaunti ya Google aliyoweka mtumiaji. Mara nyingi, huduma za Google Play zitafikia data ndani kwenye kifaa bila kukusanya data kutoka nje mwa kifaa.
Ili kusaidia kila mojawapo ya vipengele vilivyoelezwa hapo juu, huduma za Google Play zinaweza kukusanya maelezo kwa sababu zifuatazo:
Usalama na ulinzi dhidi ya ulaghai
Google hukusanya data kupitia huduma za Google Play ili kusaidia kuwekea ulinzi watumiaji, huduma za Google na programu na huduma za wasanidi programu wengine dhidi ya ulaghai, barua taka na matumizi mabaya. Hii ni pamoja na:
- Maelezo ya kuthibitisha kuwa ombi linatoka kwa mtumiaji halisi na maelezo kuhusu programu zilizowekwa, ikiwa ni pamoja na matokeo ya uchanganuzi wa programu hasidi.
- Akaunti ya Google na maelezo ya kuingia katika akaunti iwapo mtumiaji ameingia katika akaunti kwenye kifaa au amehamishia data yake kwenye kifaa kipya.
- Huenda Google ikakusanya namba ya simu ya kifaa ili kutoa huduma za kurejesha uwezo wa kufikia akaunti na kuwasajili watumiaji katika huduma zinazotegemea namba za simu (kama vile Google Meet).
- Vitambulishi vya maunzi kama vile IMEI, anwani za MAC na namba za ufuatiliaji, kusasisha vifaa kwa kutumia vipengele vipya kabisa vya kurekebisha usalama na kufuatilia mienendo kwenye mfumo wa Android, kama vile muda ambao vifaa vya aina mbalimbali hutumika. Huduma ya Google ya Usanidi wa Kifaa, ambayo hukusanya data ili kuhakikisha kuwa vifaa vinaendelea kusasishwa na vinafanya kazi vizuri iwezekanavyo, ni sehemu ya huduma za Google Play.
Kusaidia na kuboresha mfumo wa Android
Kama ilivyoelezwa hapo juu, huduma za Google Play hutoa API na huduma msingi kadhaa kwenye kifaa ambazo huwezesha Android kuwa mfumo wenye vipengele vingi vilvyounganishwa. Google inaweza kukusanya data kuhusu API na huduma hizi ili kusaidia kuzitoa, kuzidumisha na kuziboresha. Kulingana na mipangilio kwenye kifaa, Google inaweza kukusanya maelezo ya ziada kuhusu kifaa. Mifano ni kama:
- Google hukusanya data ili kufahamu jinsi API hizi zinavyotumiwa na kusaidia kuhakikisha kuwa zinafanya kazi ipasavyo.
- Iwapo huduma ya Usahihi wa Kipengele cha Google cha Kutambua Mahali kitawashwa, mbali na kutoa data sahihi ya mahali kifaa kilipo, kipengele cha maelezo ya mahali kinaweza kutumika kwa njia inayoficha utambulisho wa data ili kuboresha huduma zinazotegemea mahali.
- Kidhibiti cha matumizi na uchunguzikwenye kifaa kikiwashwa, Google hukusanya maelezo kuhusu matumizi ya kifaa na jinsi kifaa kinavyofanya kazi ili kuboresha bidhaa na huduma, kama vile programu za Google na vifaa vya Android.
Kutoa huduma za Google
Mtumiaji anapotumia programu na huduma za Google kwenye Android, Google hukusanya data kupitia huduma za Google Play ili kutoa na kuboresha programu na huduma hizo. Kwa mfano:
- Kulingana na mipangilio aliyoweka mtumiaji, Google hukusanya data kama vile anwani na alamisho ili kuzisawazisha kwenye vifaa na wingu.
- Huduma za Google Play husawazisha mipangilio aliyoweka mtumiaji kwenye akaunti ya Google katika vifaa vyote na kukusanya maelezo ili kusaidia kulinda akaunti yake.
- Huduma za Google Play zinaweza kukusanya data ili kuwezesha utendaji wa programu zilizopachikwa kama vile Ramani za Google.
- Huduma za Google Play huwasaidia watumiaji kuwasiliana na kutuma ujumbe moja kwa moja kwa biashara.
- Kwa kutumia Google Pay, huduma za Google Play huwasaidia watumiaji kudhibiti maelezo yao ya malipo, kufanya malipo ya kielektroniki au kutumia ufunguo dijitali wa gari kwa usalama.
- Google hukusanya data unapotumia wasifu au huduma za Michezo ya Google Play.
- Kwa watumiaji ambao wameweka mipangilio ya “Huhifadhi shughuli zako kutoka kwa programu kwenye kifaa hiki” katika kipengele cha Historia ya Shughuli kwenye Wavuti na Programu katika vifaa vyao, Google inaweza kuhifadhi data ya shughuli kutoka kwa programu zilizo katika kifaa kwenye Akaunti yao ya Google ili iweze kutumika kuweka mapendeleo katika programu na huduma za Google.