Ruhusa na API Zinazofikia Maelezo Nyeti

Tutafanya mabadiliko kwenye makala haya

Makala haya yatasasishwa ili kuonyesha mabadiliko yaliyotangazwa hivi majuzi.

Kwa hali ya utumiaji inayodumisha faragha ya watumiaji, tunawaletea sera ya Ruhusa za Picha na Video ili kupunguza idadi ya programu zinazoruhusiwa kuomba ruhusa pana za picha/video (READ_MEDIA_IMAGES na READ_MEDIA_VIDEO). Programu zinaweza tu kufikia picha na video kwa madhumuni yanayohusiana moja kwa moja na utendaji wa programu. Programu ambazo zinahitaji kufikia faili hizi mara moja tu au mara chache zinaombwa kutumia kiteuzi cha mfumo, kama vile kiteua picha cha Android. (kuanzia Tarehe 31 Agosti, 2024)

Tunasasisha Sera ya Health Connect ili kurahisisha mchakato wa kutuma maombi wa Health Connect pamoja na kutii sera ya Programu za Afya. Baadye mwaka huu, taarifa mpya ya Dashibodi ya Google Play itatumika badala ya mchakato uliopo wa kutumia fomu. (kuanzia Tarehe 31 Agosti, 2024)

Ili ukague makala yaliyosasishwa ya "Ruhusa na API Zinazofikia Taarifa Nyeti", tembelea ukurasa huu.

Maombi ya ruhusa na API zinazofikia maelezo nyeti lazima ziwe bayana kwa mtumiaji. Unapaswa tu kuomba ruhusa na API zinazofikia maelezo nyeti zinazohitajika kutekeleza vipengele au huduma za sasa katika programu yako ambazo umezitangaza kwenye ukurasa wa programu yako katika Google Play. Hupaswi kutumia ruhusa au API zinazofikia maelezo nyeti ambazo zinakupa ufikiaji wa data ya vifaa au ya watumiaji kwa madhumuni yasiyofichuliwa, yasiyotekelezwa au yasiyoruhusiwa au kwenye vipengee ambavyo haviruhusiwi. Huruhusiwi kuuza wala kushiriki data binafsi au nyeti inayofikiwa kupitia ruhusa au API zinazoweza kufikia maelezo nyeti.

Omba ruhusa au API zinazofikia maelezo nyeti ili ufikie data husika (kupitia maombi endelevu), ili watumiaji waweze kuelewa kwa nini programu yako inaomba ruhusa. Tumia data kwa madhumuni ambayo mtumiaji ameidhinisha pekee. Kama ungependa kutumia data kwa madhumuni mengine baadaye, lazima uwaombe watumiaji idhini na uhakikishe wanakubali kabisa matumizi ya ziada.

Ruhusa Zinazodhibitiwa

Mbali na maelezo yaliyo hapo juu, ruhusa zinazodhibitiwa ni ruhusa ambazo zimebainishwa kuwa Hatari, Maalum,  Saini au jinsi inavyobainishwa hapa chini. Ruhusa hizi zinategemea vidhibiti na masharti ya ziada yafuatayo:

  • Data ya kifaa au ya mtumiaji inayofikiwa kupitia Ruhusa Zilizodhibitiwa inachukuliwa kuwa data nyeti na binafsi. Masharti ya Sera ya Data ya Mtumiaji yatatumika.
  • Heshimu uamuzi wa watumiaji iwapo watakataa ombi la kutoa Ruhusa Inayodhibitiwa na watumiaji hawapaswi kulazimishwa au kulaghaiwa ili watoe idhini ya ruhusa zozote zisizo muhimu. Ni lazima ujitahidi kuwakubali watumiaji ambao hawatoi uwezo wa kufikia ruhusa nyeti (kwa mfano, kumruhusu mtumiaji aweke mwenyewe nambari ya simu iwapo hajaruhusu ufikiaji wa Rekodi ya Nambari za Simu).
  • Haturuhusu kabisa matumizi ya ruhusa kwa njia inayokiuka sera za programu hasidi za Google Play (ikiwa ni pamoja na Matumizi Mabaya ya Ufikiaji Maalum).

Ruhusa fulani Zinazodhibitiwa zinaweza kutegemea masharti ya ziada jinsi inavyoelezewa kwa kina hapa chini. Lengo la masharti haya ni kulinda faragha ya mtumiaji. Tunaweza kuruhusu hali kadhaa zisizofuata masharti yaliyo hapa chini katika matukio ambayo hutokea kwa nadra, ambapo programu zinatoa kipengele cha lazima au muhimu zaidi na katika hali ambapo hakuna njia mbadala ya kutoa kipengele hicho. Tunatathmini hali pendekezwa zisizofuata kanuni kwa kuzingatia uwezekano wa kuathiri faragha au usalama wa watumiaji.

 

Ruhusa za SMS na Rekodi ya Nambari za Simu

Ruhusa za SMS na Rekodi ya Nambari za Simu huchukuliwa kuwa data ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi kwa mujibu wa sera ya Taarifa Binafsi na Nyeti na masharti yafuatayo:

Ruhusa Zinazodhibitiwa Masharti
Kikundi cha ruhusa za Rekodi ya Nambari za Simu (k.m. READ_CALL_LOG, WRITE_CALL_LOG, PROCESS_OUTGOING_CALLS) Sharti iwe imesajiliwa kikamilifu kuwa kidhibiti chaguomsingi cha Simu au Programu ya Mratibu kwenye kifaa.
Kikundi cha ruhusa za SMS (k.m. READ_SMS, SEND_SMS, WRITE_SMS, RECEIVE_SMS, RECEIVE_WAP_PUSH, RECEIVE_MMS) Sharti iwe imesajiliwa kikamilifu kuwa kidhibiti chaguomsingi cha SMS au Programu ya Mratibu kwenye kifaa.

 

Programu zisizo na uwezo wa kidhibiti chaguomsingi cha SMS, Simu au Programu ya Mratibu hazipaswi kutangaza matumizi ya ruhusa zilizo hapo juu kwenye faili ya maelezo. Uwezo huu unajumuisha maandishi ya kishikilia nafasi kwenye faili ya maelezo. Vile vile, ni lazima programu ziwe zimesajiliwa kuwa kidhibiti chaguomsingi cha programu ya Mratibu, SMS au Simu kabla ya kudokezea watumiaji wakubali mojawapo ya ruhusa zozote zilizo hapo juu na sharti ziache mara moja kutumia ruhusa zikiacha kuwa kidhibiti chaguomsingi. Matumizi na hali zisizofuata kanuni zinazoruhusiwa zinapatikana kwenye ukurasa huu wa Kituo cha Usaidizi.

Programu zinaweza kutumia tu ruhusa (na data yoyote inayotokana na ruhusa) ili kutoa utendaji wa msingi wa programu ulioidhinishwa. Utendaji wa msingi unafafanuliwa kuwa lengo kuu la programu. Hili linaweza kujumuisha vipengele vya msingi, ambavyo vinapaswa kurekodiwa kwa njia dhahiri katika maelezo ya programu. Bila vipengele vya msingi, programu “haijakamilika” au inachukuliwa kuwa haiwezi kutumika. Uhamishaji, kushiriki au matumizi yaliyoidhinishwa ya data hii ni sharti yatoe tu huduma au vipengele vya msingi katika programu na matumizi yake hayapaswi kuenezwa kwa madhumuni mengine yoyote (k.m. madhumuni ya utangazaji au uuzaji, kuboresha programu au huduma nyingine). Hupaswi kutumia njia mbadala (ikiwa ni pamoja na ruhusa, API au vyanzo vya wengine) ili kupata data inayohusishwa na ruhusa za SMS au Rekodi ya Nambari za Simu.

 

Ruhusa za Mahali

Data ya mahali kifaa kilipo huchukuliwa kuwa data ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi kwa mujibu wa sera ya Taarifa Binafsi na Nyeti na Sera ya Ruhusa ya Kubainisha Mahali Chinichini na masharti yafuatayo:

  • Programu hazipaswi kufikia data inayolindwa kwa ruhusa za mahali (k.m., ACCESS_FINE_LOCATION, ACCESS_COARSE_LOCATION, ACCESS_BACKGROUND_LOCATION) baada ya kutohitajika tena kutekeleza huduma au vipengele vya sasa katika programu yako.
  • Usiwahi kuomba ruhusa za mahali kutoka kwa watumiaji kwa lengo kuu la kuonyesha matangazo au takwimu. Programu ambazo zinaendeleza matumizi yanayoruhusiwa ya data hii kwa kuonyesha matangazo ni lazima zitii Sera yetu ya Matangazo.
  • Programu zinapaswa kuomba kiwango cha chini zaidi kinachohitajika cha ufikiaji (yaani, cha juujuu badala ya kuwa ya kina, na ufikiaji wakati programu inatumika badala ya chinichini) ili kutoa kipengele au huduma ya sasa inayotaka data ya mahali na watumiaji wanapaswa kutarajia kuwa kipengele au huduma hiyo inahitaji kiwango cha data ya mahali kilichoombwa. Kwa mfano, tunaweza kukataa programu zinazoomba au kufikia data ya mahali chinichini bila kutoa sababu za kutosha.
  • Ufikiaji wa data ya mahali chinichini unapaswa tu kutumika kutoa vipengele muhimu kwa mtumiaji na vinavyohusiana na utendakazi wa msingi wa programu.

Programu zinaruhusiwa kufikia data ya mahali kwa kutumia ruhusa ya huduma ya ufikiaji wakati programu inatumika (programu ina uwezo wa ufikiaji wakati inatumika tu, k.m., "inapotumika") ikiwa matumizi haya:

  • yameanzishwa kuendeleza kitendo cha ndani ya programu kilichoanzishwa na mtumiaji na
  • yanasimamishwa mara moja baada ya programu kukamilisha matumizi yaliyokusudiwa na kitendo kilichoanzishwa na mtumiaji.

Ni lazima programu zilizobuniwa kwa ajili ya watoto zitii sera ya Programu za Familia Yote.

Ili upate maelezo zaidi kuhusu masharti ya sera, tafadhali angalia makala haya ya usaidizi.

 

Ruhusa ya Kufikia Faili Zote

Sifa za faili na saraka kwenye kifaa cha mtumiaji huchukuliwa kuwa data ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi kwa mujibu wa sera ya Taarifa Binafsi na Nyeti na masharti yafuatayo:

  • Programu zinapaswa tu kuomba idhini ya kufikia hifadhi ya kifaa kwa namna ambayo inahitajika ili programu ifanye kazi na hazipaswi kuomba idhini ya kufikia hifadhi ya kifaa kwa niaba ya programu yoyote ya wengine kwa madhumuni yoyote ambayo hayahusiani na utendaji ulio muhimu kwa mtumiaji katika programu.
  • Vifaa vya Android vinavyotumia toleo la R au matoleo mapya, vitahitaji ruhusa ya MANAGE_EXTERNAL_STORAGE ili kudhibiti idhini ya kufikia hifadhi inayoshirikiwa. Ni lazima programu zote zinazolenga toleo la R na zinazoomba idhini ya kufikia hifadhi iliyoshirikiwa (“Ufikiaji wa faili zote”) zipite ukaguzi unaofaa wa ufikiaji kabla ya kuchapishwa. Ni lazima programu zinazokubaliwa kutumia ruhusa hii ziwaombe watumiaji kwa njia ya wazi kuwasha kipengele cha “Ufikiaji wa faili zote” kwenye programu yao chini ya mipangilio ya “Ufikiaji maalum wa programu”. Ili upate maelezo zaidi kuhusu masharti ya R, tafadhali angalia makala haya ya usaidizi.

 

Ruhusa ya Uonekanaji wa Kifurushi (Programu)

Orodha ya programu zilizosakinishwa iliyotumwa kutoka kwenye kifaa huchukuliwa kuwa data ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi kwa mujibu wa sera ya Maelezo Nyeti na ya Kibinafsi  na masharti yafuatayo:

Programu ambazo zina lengo kuu la kufungua, kutafuta au kufanya kazi na programu zingine kwenye kifaa, zinaweza kupata ruhusa inayofaa upeo wa uonekanaji kwenye programu zingine zilizosakinishwa kwenye kifaa jinsi inavyobainishwa hapa chini:

  • Uonekanaji mpana wa programu: Uonekanaji mpana ni uwezo wa programu wa kuona kwa kina (au “upana”) programu zilizosakinishwa ("vifurushi") kwenye kifaa.
    • Kwa programu zinazolenga API ya kiwango cha 30 au cha juu, uonekanaji mpana kwenye programu zilizosakinishwa kupitia ruhusa ya QUERY_ALL_PACKAGES unatekelezwa tu katika matumizi mahususi ambapo ufahamu na/au uwezo wa kufanya kazi pamoja na programu yoyote au zote kwenye kifaa unahitajika ili programu ifanye kazi. 
    • Matumizi ya njia mbadala za kukadiria kiwango cha uonekanaji mpana zinazohusishwa na ruhusa ya QUERY_ALL_PACKAGES pia yanatekelezwa tu kwenye utendakazi wa msingi wa programu inayotumiwa na mtumiaji na uwezo wa kufanya kazi pamoja na programu zozote zilizogunduliwa kupitia njia hii.
    • Tafadhali angalia makala haya ya Kituo cha Usaidizi ili ujue hali za matumizi yanayoruhusiwa katika ruhusu ya QUERY_ALL_PACKAGES.
  • Uonekanaji mdogo wa programu: Uonekanaji mdogo wa programu ni wakati ambapo programu inapunguza uwezo wa kufikia data kwa kutuma hoja za programu mahususi kutumia njia zinazolengwa zaidi (badala ya “pana”) (k.m. kutuma hoja za programu mahususi ambazo zinatimiza taarifa ya faili ya maelezo ya programu yako). Unaweza kutumia njia hii ili kutuma hoja za programu katika hali ambapo programu yako ina uwezo wa kufanya kazi na programu zingine unaotii sera au kudhibiti programu hizi. 
  • Ni lazima uonekanaji kwenye orodha ya programu zilizosakinishwa kwenye kifaa uhusiane moja kwa moja na lengo kuu au utendakazi wa msingi ambao watumiaji hufikia ndani ya programu yako. 

Hupaswi kuuza au kushiriki data ya orodha ya programu iliyotumwa kutoka kwenye programu zinazosambazwa na Google Play kwa ajili ya takwimu au madhumuni ya uchumaji wa mapato ya matangazo.

 

API ya Ufikivu

API ya Ufikivu haitumiki:

  • Kubadilisha mipangilio ya mtumiaji bila ruhusa yake au zuia uwezo wa mtumiaji kuzima au kuondoa huduma au programu yoyote isipokuwa inapoidhinishwa na mzazi au mlezi kupitia programu ya kidhibiti cha wazazi au wasimamizi walioidhinishwa kupitia programu ya usimamizi wa biashara; 
  • Kukwepa vidhibiti vya faragha na arifa vilivyojumuishwa kwenye Android; au
  • Kubadilisha au kutumia kiolesura kwa udanganyifu au vinginevyo kwa njia inayokiuka Sera za Wasanidi Programu katika Google Play. 

API ya Ufikivu haijabuniwa na haiwezi kuombwa kwa ajili ya kurekodi simu ya sauti kutoka mbali. 

Ni lazima utumiaji wa API ya Ufikivu urekodiwe kwenye ukurasa wa programu katika Google Play.

Mwongozo wa IsAccessibilityTool

Programu ambazo utendaji wa msingi unanuia kuwasaidia walemavu kwa njia ya moja kwa moja zinatimiza masharti ya kutumia IsAccessibilityTool ili ziweze kujibainisha hadharani inavyofaa kuwa programu za ufikivu.

Programu zisizotimiza masharti ya IsAccessibilityTool hazipaswi kutumia kitia alama na lazima zitimize masharti muhimu ya ufumbuzi na idhini kama inavyobainishwa katika Sera ya Data ya Mtumiaji kwa vile utendaji unaohusiana na ufikivu si bayana kwa mtumiaji. Tafadhali rejelea makala ya kituo cha usaidizi ya API ya Huduma ya Ufikivu ili upate maelezo zaidi.

Ni lazima programu zitumie API na ruhusa zinazohusisha vipengele vichache zaidi badala ya API ya Ufikivu inapowezekana ili kufikia utendaji unaohitajika. 

 

Omba Ruhusa ya Kusakinisha Vifurushi

Ruhusa hii ya REQUEST_INSTALL_PACKAGES inaruhusu programu kuomba usakinishaji wa vifurushi vya programu.​​ Ili utumie ruhusa hii, utendaji wa msingi wa programu yako lazima ujumuishe:

  • Kutuma au kupokea vifurushi vya programu; na
  • Kuruhusu usakinishaji wa vifurushi vya programu unaoanzishwa na mtumiaji.

Utendaji unaoruhusiwa unajumuisha:

  • Kuvinjari au kutafuta katika wavuti
  • Huduma za mawasiliano zinazoruhusu viambatisho
  • Kushiriki, kuhamisha au kudhibiti faili
  • Kudhibiti kifaa cha kampuni
  • Kuhifadhi nakala au kurejesha vipengee
  • Uhamishaji kwenye Kifaa au Simu
  • Programu inayotumika kudhibiti Jam inayosawazisha simu na kifaa cha kuvaliwa au kifaa cha IoT (kwa mfano, saa mahiri au televisheni inayoweza kuunganisha kwenye intaneti)

Utendaji wa msingi unafafanuliwa kuwa ni lengo kuu la programu. Utendaji wa msingi, pamoja na vipengele vyovyote vya msingi vinavyojumuisha utendaji huu wa msingi lazima vitangazwe na kuonyeshwa kwa njia dhahiri kwenye maelezo ya programu.

Huruhusiwi kutumia REQUEST_INSTALL_PACKAGES kufanya masasisho binafsi, marekebisho au kuunganisha APK nyingine kwenye faili ya kipengee isipokuwa kwa madhumuni ya usimamizi wa kifaa. Masasisho yote au usakinishaji wa vifurushi ni lazima zitii sera ya Google Play Dhidi ya Matumizi Mabaya ya Vifaa na Mtandao na lazima zianzishwe na ziendeshwe na mtumiaji.

 

Ruhusa za Health Connect kutoka Android

Data inayofikiwa kupitia Ruhusa za Health Connect huchukuliwa kuwa data ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi kwa mujibu wa sera ya Data ya Mtumiaji na masharti ya ziada yafuatayo:

Ufikiaji na Matumizi Sahihi ya Health Connect

Maombi ya kufikia data kupitia Health Connect lazima yawe dhahiri na yanaeleweka. Health Connect inapaswa tu kutumika kwa mujibu wa sera, sheria na masharti yanayotumika pamoja na hali zilizoidhinishwa, kama ilivyobainishwa katika sera hii. Hatua hii inamaanisha kwamba unapaswa tu kuomba idhini ya kufikia ruhusa wakati programu au huduma yako itatimiza moja kati ya hali za matumizi zilizoidhinishwa.

Hali za matumizi zilizoidhinishwa ili kufikia Ruhusa za Health Connect ni:

  • Programu au huduma zenye kipengele kimoja au zaidi chenye manufaa kwa afya na siha ya mtumiaji kupitia kiolesura kinachoruhusu moja kwa moja watumiaji waweke rekodi zao za kila siku, kuripoti, kufuatilia na/au kuchanganua mazoezi yao ya mwili, kulala, ustawi wa akili, lishe, vipimo vya afya, maelezo ya kimaumbile na/au maelezo mengine yanayohusiana na afya au siha pamoja na vipimo.
  • Programu au huduma zenye kipengele kimoja au zaidi chenye manufaa kwa afya na siha ya mtumiaji kupitia kiolesura kinachoruhusu watumiaji wahifadhi mazoezi yao ya mwili, kulala, ustawi wa akili, lishe, vipimo vya afya, maelezo ya kimaumbile na/au maelezo mengine yanayohusiana na afya au siha pamoja na vipimo kwenye simu na/au kifaa chao cha kuvaliwa na kushiriki data yao na programu zingine kwenye kifaa zinazotimiza hali hizi za matumizi.

Health Connect ni mfumo wa madhumuni ya jumla wa kuhifadhi na kushiriki data ambao huruhusu watumiaji wakusanye data ya afya na siha kutoka vyanzo mbalimbali kwenye kifaa chao cha Android kisha kushiriki na wengine watakapoamua. Data huenda ikatoka kwenye vyanzo mbalimbali kama itakavyoamuliwa na watumiaji. Wasanidi programu wanapaswa kutathmini iwapo Health Connect ni sahihi kwa matumizi wanayokusudia na kuchunguza pamoja na kuhakiki chanzo na ubora wa data yoyote kutoka Health Connect inayohusiana na madhumuni yoyote, hasa kwa matumizi ya utafiti, afya au tiba.

  • Programu zinazoendesha utafiti unaohusu afya wenye washiriki ambao ni binadamu, unaotumia data kutoka Health Connect zinapaswa kupata idhini kutoka kwa washiriki au ikiwa washiriki ni watoto, idhini kutoka kwa mzazi au mlezi. Idhini hii inapaswa kujumuisha (a) aina, madhumuni na muda wa utafiti; (b) utaratibu, hatari na manufaa kwa mshiriki; (c) maelezo kuhusu usiri na ushughulikiaji wa data (ikiwa ni pamoja na ushiriki wowote na wengine); (d) mtu wa kuwasiliana naye endapo kuna maswali kutoka kwa mshiriki; na (e) mchakato wa kujiondoa. Programu zinazoendesha utafiti unaohusu afya yenye washiriki ambao ni binadamu, unaotumia data kutoka Health Connect zinapaswa kupata idhini kutoka bodi ya kujitegemea yenye lengo la 1) kulinda haki, usalama na ustawi wa washiriki na 2) yenye mamlaka ya kuchunguza, kubadilisha na kuidhinisha utafiti wenye washiriki ambao ni binadamu. Ushahidi wa uthibitisho unapaswa kutolewa utakapohitajika.
  • Pia, ni jukumu lako kuhakikisha kwamba unatii mahitaji yoyote ya mamlaka za usimamizi au sheria ambazo huenda zikatumika kulingana na matumizi uliyokusudia ya Health Connect pamoja na data yoyote kutoka Health Connect. Isipokuwa kama ilivyobainishwa dhahiri katika lebo au taarifa zilizotolewa na Google kwa bidhaa na huduma mahususi za Google, Google haiidhinishi matumizi ya au kuthibitisha usahihi wa data yoyote iliyo katika Health Connect kwa matumizi na madhumuni yoyote, hasa, kwa matumizi ya utafiti, afya au tiba. Google inakanusha dhima zote zinazohusiana na matumizi ya data inayopatikana kupitia Health Connect.

Matumizi yaliyowekewa Vizuizi

Unapotumia Health Connect kwa matumizi yanayofaa, matumizi yako ya data iliyofikiwa kupitia Health Connect pia yanapaswa kutii masharti yaliyo hapa chini. Masharti haya yanatumika kwenye data ghafi iliyopatikana kutoka Health Connect pamoja na data iliyojumlishwa, isiyomtambulisha mtu au iliyotokana na data hiyo ghafi.

  • Fanya utumiaji wako wa data ya Health Connect uwe tu kwa ajili ya utoaji au uboreshaji wa hali yako ya matumizi yanayofaa au vipengele vinavyoonekana na ni dhahiri katika kiolesura cha programu inayoomba.
  • Hamishia tu kwa wengine data ya mtumiaji:
    • Ili kutoa au kuboresha hali yako ya matumizi yanayofaa au vipengele ambavyo vipo dhahiri katika kiolesura cha programu inayoomba na kwa idhini ya mtumiaji pekee;
    • Kwa madhumuni ya usalama, ikiwa ni lazima (kwa mfano, kuchunguza matumizi mabaya);
    • Ili kutii sheria na/au kanuni zinazotumika; au,
    • Kama sehemu ya muungano wa kibiashara, ununuzi wa biashara au kuuza mali za msanidi programu baada ya kupata idhini dhahiri ya awali kutoka kwa mtumiaji.
  • Usiruhusu binadamu asome data ya mtumiaji, isipokuwa:
    • Idhini dhahiri ya kusoma data mahususi imetolewa na mtumiaji;
    • Ni lazima kwa madhumuni ya usalama, (kwa mfano, kuchunguza matumizi mabaya);
    • Ili kutii sheria zinazotumika; au,
    • Data (ikiwa ni pamoja na data iliyotokana na data ghafi) inajumlishwa na kutumika katika shughuli za ndani kwa mujibu wa mahitaji ya faragha pamoja na mahitaji mengine ya kisheria yanayotumika katika eneo la mamlaka.

Uhamishaji, matumizi au uuzaji mwingine wowote wa data ya Health Connect hauruhusiwi, ikiwa ni pamoja na:

  • Kuhamisha au kuuza data ya mtumiaji kwenda kwa wengine kama vile mifumo ya utangazaji, madalali wa data au wauzaji wowote wa taarifa.
  • Kuhamisha, kuuza au kutumia data ya mtumiaji ili kuonyesha matangazo, ikijumuisha matangazo yaliyowekewa mapendeleo au yanayotegemea mambo yanayomvutia mtumiaji.
  • Kuhamisha, kuuza au kutumia data ya mtumiaji ili kubaini ustahili wa mikopo au kwa madhumuni ya kukopesha.
  • Kuhamisha, kuuza au kutumia data ya mtumiaji na bidhaa au huduma yoyote inayoweza kutimiza masharti ya kuwa kifaa cha matibabu kwa mujibu wa Kifungu cha 201(h) cha Sheria ya Marekani ya Chakula, Dawa na Vipodozi iwapo data ya mtumiaji itatumiwa na kifaa cha matibabu ili kutekeleza utendaji wake uliodhibitiwa.
  • Kuhamisha, kuuza au kutumia data ya mtumiaji kwa madhumuni yoyote au kwa njia yoyote inayohusu Maelezo ya Afya Yaliyolindwa (kama ilivyobainishwa na HIPAA) isipokuwa endapo ulipokea idhini kwa maandishi hapo awali kutoka Google kwa ajili ya matumizi hayo.

Uwezo wa kufikia Health Connect haupaswi kutumika kinyume cha sera hii au sera pamoja na sheria na masharti mengine ya Health Connect yanayotumika, ikiwa ni pamoja na madhumuni yafuatayo:

  • Usitumie Health Connect kusanidi au kujumuisha katika, programu, mazingira au shughuli ambazo matumizi au kutokufanikiwa kwa Health Connect huenda kukatarajiwa kusababisha kifo, majeraha ya mwili au uharibifu wa mali au mazingira (kama vile utengenezaji au uendeshaji wa vituo vya nyuklia, udhibiti wa safari za ndege, mifumo ya kusaidia kuokoa uhai au ya silaha).
  • Usifikie data yoyote iliyopatikana kupitia Health Connect kwa kutumia programu zisizokuwa na kiolesura. Ni lazima programu zionyeshe aikoni inayotambulika vizuri kwenye trei ya programu, mipangilio ya programu ya kifaa, aikoni za arifa, n.k.
  • Usitumie Health Connect na programu zinazosawazisha data kati ya vifaa au mifumo isiyooana.
  • Health Connect haiweza kuunganisha kwenye programu, huduma au vipengele ambavyo vinalenga watoto pekee. Health Connect haijaidhinishwa kwa ajili ya huduma zinazolenga watoto.

Taarifa ya kuidhinisha kwamba matumizi yako ya data ya Health Connect yanatii vikwazo vya Matumizi yaliyowekewa Vizuizi inapaswa ifichuliwe katika programu yako au kwenye tovuti inayomilikiwa na huduma yako ya wavuti au programu; kwa mfano, kiungo katika ukurasa wa kwanza kinachoelekeza kwenye ukurasa maalumu au sera ya faragha inayosema: "Matumizi ya taarifa kutoka Health Connect yanatii sera ya Ruhusa za Health Connect, ikiwa ni pamoja na masharti ya Matumizi yaliyowekewa Vizuizi."

Upeo wa kiwango cha chini

Unaweza tu ukaomba idhini ya kufikia ruhusa ambazo ni muhimu kwenye utekelezaji wa programu au utendaji wa huduma yako. 

Hatua hii inamaanisha:

  • Usiombe idhini ya kufikia maelezo ambayo huyahitaji. Omba tu idhini ya kufikia ruhusa ambazo zinahitajika ili kutekeleza vipengele au huduma za bidhaa yako. Ikiwa bidhaa yako haihitaji kufikia ruhusa mahususi, hupaswi kuomba idhini ya kufikia ruhusa hizi.

Ilani Wazi na Sahihi pamoja na Udhibiti

Health Connect hushughulikia data ya afya na siha, inayojumuisha maelezo nyeti na ya binafsi. Programu na huduma zote lazima zijumuishe sera ya faragha, inayopaswa kufumbua kwa kina jinsi programu au huduma yako inavyokusanya, kutumia na kushiriki data ya mtumiaji. Hatua hii inajumuisha aina ya washirika ambao hutumiwa data ya mtumiaji, jinsi unavyotumia data, jinsi unavyoihifadhi na kuilinda na kuhusu kile kinachofanyika kwenye data iwapo akaunti itafungwa na/au kufutwa.

Mbali na masharti yaliyo chini ya sheria inayotumika, unapaswa pia utii masharti yafuatayo:

  • Ni sharti utoe ufumbuzi kuhusu jinsi unavyoifikia data, kuikusanya, kuitumia na kuishiriki. Ufumbuzi huo:
    • Ni lazima uwakilishe kwa usahihi utambulisho wa programu au huduma inayotaka iwe na uwezo wa kufikia data ya mtumiaji;
    • Ni lazima utoe maelezo sahihi na yaliyodhahiri yanayofafanua aina za data inayofikiwa, inayoombwa na/au inayokusanywa;
    • Ni lazima ufafanue jinsi data itakavyotumika na/au kushirikiwa: Ikiwa utaomba data kwa sababu moja, lakini data hiyo pia ikatumika kwa sababu ya pili, unapaswa kuwaarifu watumiaji kuhusu hali zote mbili za matumizi.
  • Ni sharti utoe hati ya usaidizi kwa mtumiaji inayoeleza jinsi watumiaji wanaweza kudhibiti na kufuta data yao kutoka kwenye programu yako.

Kushughulikia Data kwa Usalama

Unapaswa kushughulikia kwa usalama data yote ya mtumiaji. Chukua hatua adilifu na zinazofaa ili kulinda programu na mifumo yote inayotumia Health Connect dhidi ya ufikiaji, ubadilishaji, ufumbuzi, kupotea, kuharibiwa, au matumizi kwa njia isiyoidhinishwa au inayokiuka sheria.

Mbinu za usalama zinazopendekezwa hujumuisha utekelezaji na udumishaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Usalama wa Taarifa kama ilivyoainishwa kwenye ISO/IEC 27001 pamoja na kuhakikisha kwamba programu au huduma yako ya wavuti ipo imara na haina matatizo ya kawaida ya usalama kama yalivyobainishwa na OWASP Top 10.

Kulingana na API inayofikiwa pamoja na idadi ya ruhusa zilizotolewa kwa mtumiaji au watumiaji, tutahitaji programu au huduma yako ipitie tathmini ya usalama ya mara kwa mara na ipokee Barua ya Tathmini kutoka kwa wahusika wengine waliyobainishwa ikiwa bidhaa yako inahamisha data kutoka kwenye kifaa cha mtumiaji.

Kwa maelezo zaidi kuhusu masharti ya programu zinazounganisha kwenye Health Connect, tafadhali angalia makala haya ya usaidizi.

 

Huduma ya VPN

VpnService ni daraja la msingi kwa ajili ya programu kuendeleza na kutengeneza huduma yazo zenyewe za VPN. Programu zinazotumia VpnService tu, ambazo pia zina utendaji wa msingi wa VPN ndizo zinaweza kuunda njia salama ya upitishaji wa data kwenye seva ya mbali katika kifaa chenyewe. Hali zisizofuata kanuni hujumuisha programu zinazohitaji seva ya mbali kwa ajili ya utendaji wa msingi kama vile:

  • Programu za vidhibiti vya wazazi na udhibiti wa kibiashara.
  • Ufuatiliaji wa matumizi ya programu.
  • Programu za usalama wa kifaa (kwa mfano, kingavirusi, kidhibiti cha vifaa vya mkononi, kinga mtandao).
  • Zana zinazohusiana na mtandao (kwa mfano, ufikiaji wa mbali).
  • Programu za kuvinjari kwenye wavuti.
  • Programu za mtoa huduma zinazohitaji kutumia utendaji wa VPN ili kutoa huduma za simu na muunganisho.

VpnService haiwezi kutumika:

  • Kukusanya data binafsi na nyeti ya mtumiaji bila ufumbuzi dhahiri na idhini.
  • Kuelekeza kwingine au kubadilisha shughuli za mtumiaji kutoka programu zingine kwenye kifaa kwa madhumuni ya uchumaji wa mapato (kwa mfano, kufanya ionekane kuwa mtumiaji ameangalia matangazo akiwa kwenye nchi tofauti na aliyopo).

Programu zinazotumia VpnService zinapaswa:

 

Ruhusa ya Kengele Sahihi

Ruhusa mpya itakayoongezwa ya USE_EXACT_ALARM, itazinduliwa ambayo itatoa uwezo wa kufikia utendaji sahihi wa kengele katika programu kuanzia Android 13 (kiwango lengwa cha API 33). 

USE_EXACT_ALARM ni ruhusa inayodhibitiwa na programu zinapaswa tu kubainisha ruhusa hii ikiwa utendaji wake wa msingi unaonyesha hitaji la kufikia utendaji sahihi wa kengele. Programu zitakazoomba ruhusa hii inayodhibitiwa, zitakaguliwa na zile ambazo hazitatimiza kigezo cha hali ya matumizi yanayokubalika hazitaruhusiwa kuchapisha kwenye Google Play.

Hali za matumizi zinazokubalika kutumia Ruhusa ya Kengele Sahihi

Programu yako inapaswa tu kutumia utendaji wa USE_EXACT_ALARM wakati utendaji msingi wa programu yako kwa mtumiaji unahitaji vitendo vinavyolingana kwa usahihi na saa, kama vile:

  • Ni programu ya kengele au ya kupima muda.
  • Ni programu ya kalenda inayoonyesha arifa za tukio.

Ukiwa una hali ya matumizi kwa ajili ya utendaji sahihi wa kengele ambayo haipo hapa juu, unapaswa kutathmini iwapo unaweza kutumia SCHEDULE_EXACT_ALARM kama chaguo mbadala.

Ili upate maelezo zaidi kuhusu utendaji sahihi wa kengele, tafadhali angalia mwongozo huu wa msanidi programu.

 

Ruhusa ya Utaratibu wa Kuratibu Skrini Nzima

Kwa programu zinazolenga toleo la Android 14 (kiwango lengwa cha API 34) na zaidi, USE_FULL_SCREEN_INTENT ni ruhusa ya ufikiaji wa programu maalum. Programu zitaruhusiwa tu kiotomatiki kutumia ruhusa ya USE_FULL_SCREEN_INTENT ikiwa utendaji wa msingi wa programu unapatikana chini ya moja ya aina zilizo hapa chini zinazohitaji arifa za kipaumbele cha juu:

  • kuweka kengele
  • kupokea simu zinazopigwa au simu za video

Programu zinazoomba ruhusa hii zitakaguliwa na zile ambazo hazitimizi kigezo cha hapo juu hazitapewa ruhusa hii kiotomatiki. Kwa hivyo, lazima programu ziombe ruhusa kutoka kwa mtumiaji ili kutumia USE_FULL_SCREEN_INTENT.

Kama kikumbusho, matumizi yoyote ya ruhusa ya USE_FULL_SCREEN_INTENT lazima yatii Sera zote za Google Play za Wasanidi Programu, ikiwa ni pamoja na sera za Programu za Simu Zisizotakikana, Matumizi Mabaya ya Kifaa na Mtandao na Matangazo. Arifa za utaratibu wa kuratibu skrini nzima hazipaswi kuathiri, kukatiza, kuharibu au kufikia kifaa cha mtumiaji kwa njia ambayo haijaidhinishwa. Pia, programu hazipaswi kuathiri programu nyingine au urahisi wa kutumia kifaa.

Pata maelezo zaidi kuhusu ruhusa ya USE_FULL_SCREEN_INTENT katika Kituo chetu cha Usaidizi.

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Menyu kuu
6391720711131771556
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
true
true
true
true
true
92637
false
false