Ni lazima uwe muwazi unaposhughulikia data ya watumiaji (kwa mfano, maelezo yanayokusanywa kutoka kwa mtumiaji au kuhusu mtumiaji ikiwa ni pamoja na maelezo ya kifaa). Hii inamaanisha kufumbua uwezo wa kufikia kukusanya, kutumia, kushughulikia na kushiriki data ya mtumiaji kutoka kwenye programu yako na kudhibiti matumizi ya data kwa madhumuni ya kutii sera yaliyofumbuliwa. Tafadhali kumbuka kuwa kushughulikia data yoyote nyeti au binafsi ya mtumiaji pia hutegemea masharti ya ziada katika sehemu ya "Data Binafsi na Nyeti ya Mtumiaji" hapo chini. Masharti haya ya Google Play yanatumika pamoja na masharti yoyote yanayobainishwa na sheria husika za faragha na ulinzi wa data.
Ikiwa unajumuisha msimbo wa wahusika wengine (kwa mfano, SDK) kwenye programu yako, ni lazima uhakikishe kuwa msimbo wa wahusika wengine unaotumika kwenye programu yako, na desturi za wahusika wengine kuhusiana na data ya mtumiaji, zinatii Sera za Mpango wa Wasanidi Programu wa Google Play, ambazo zinajumuisha matumizi na masharti ya ufumbuzi. Kwa mfano, ni lazima uhakikishe kuwa watoa huduma wako wa SDK hawauzi data nyeti ya mtumiaji kwenye programu yako. Masharti haya yanatumika bila kujali kama data ya mtumiaji inahamishwa baada ya kutumwa kwenye seva, au kwa kupachika msimbo wa wahusika wengine katika programu yako.
KUNJA ZOTE PANUA ZOTE
Data Binafsi na Nyeti ya MtumiajiData ya mtumiaji ambayo ni nyeti na ya binafsi hujumuisha, lakini si tu, taarifa binafsi inayoweza kumtambulisha mtu, maelezo ya fedha na malipo, maelezo ya uthibitishaji, orodha ya anwani, anwani, mahali kifaa kilipo, data inayohusiana na SMS pamoja na simu, data ya afya, data ya Health Connect, orodha ya programu nyinginezo zilizopo kwenye kifaa, maikrofoni, kamera na data nyingine nyeti ya matumizi au ya kifaa. Iwapo programu yako inashughulikia data nyeti na ya binafsi, ni sharti:
Masharti ya Idhini na Ufumbuzi DhahiriKatika hali ambapo uwezo wa programu yako kufikia, kukusanya, kutumia au kushiriki data nyeti na binafsi ya mtumiaji unaweza usiwe ndani ya matarajio ya mtumiaji wa bidhaa au kipengele husika (kwa mfano, ikiwa ukusanyaji wa data unafanyika chinichini wakati mtumiaji hatumii programu yako), ni lazima utimize masharti yafuatayo: Ufumbuzi dhahiri: Ni lazima utoe ufumbuzi wa ndani ya programu kuhusu jinsi unavyofikia data, kuikusanya, kuitumia na kuishiriki. Ufumbuzi wa ndani ya programu:
Idhini na ruhusa za programu inapotumika: Maombi ya idhini ya mtumiaji ya ndani ya programu na maombi ya ruhusa za programu inapotumika lazima yatanguliwe papo hapo na ufumbuzi wa ndani ya programu unaotimiza masharti ya sera hii. Ombi la programu la idhini:
Programu zinazotegemea misingi mingine ya kisheria ili kuchakata data nyeti na binafsi ya mtumiaji bila idhini, kama vile sababu halali chini ya EU GDPR, lazima zitii mahitaji yote ya kisheria yanayotumika na kutoa ufumbuzi unaofaa kwa watumiaji, ikiwa ni pamoja na ufumbuzi wa ndani ya programu kama inavyohitajika chini ya sera hii. Ili utimize masharti ya sera, inapendekezwa kwamba utumie mfano wa muundo ufuatao wa Ufumbuzi Dhahiri panapohitajika:
Ikiwa programu yako itajumuisha msimbo wa wahusika wengine (kwa mfano, SDK) ambayo imeundwa kukusanya data nyeti ya mtumiaji kwa chaguomsingi, ni lazima, ndani ya wiki 2 baada ya kupokea ombi kutoka Google Play (au ikiwa ombi la Google Play litatoa muda mrefu zaidi, ndani ya kipindi hicho), utoe ushahidi wa kutosha unaoonyesha kuwa programu yako inatimiza masharti ya Idhini na Ufumbuzi Dhahiri wa sera hii, ikijumuisha jinsi unavyofikia data, kuikusanya, kuitumia au kuishiriki kupitia msimbo wa wahusika wengine.
Rejelea kwenye makala haya ili upate maelezo zaidi kuhusu Masharti ya Idhini na Ufumbuzi Dhahiri. Masharti ya Ufikiaji wa Data Binafsi na NyetiMbali na masharti yaliyo hapo juu, jedwali lililo hapa chini linafafanua masharti ya shughuli mahususi.
|
Sehemu ya usalama wa dataLazima wasanidi programu wote wajaze kwa uwazi na usahihi sehemu ya Usalama wa data ya kila programu kwa kutoa ufafanuzi kuhusu ukusanyaji, utumiaji na kushiriki data ya mtumiaji. Msanidi programu anawajibikia usahihi wa lebo na kusasisha maelezo haya. Panapofaa, lazima sehemu hiyo ilingane na ufumbuzi uliofanywa kwenye sera ya faragha ya programu. Tafadhali rejelea makala haya ili upate maelezo ya ziada kuhusu kujaza Sehemu ya Usalama wa Data. Sera ya FaraghaNi lazima programu zote zichapishe kiungo cha sera ya faragha katika sehemu iliyobainishwa kwenye Dashibodi ya Google Play na kiungo au maandishi ya sera ya faragha ndani ya programu yenyewe. Ni lazima sera ya faragha pamoja na ufumbuzi wowote wa ndani ya programu, ifafanue kwa kina jinsi programu yako inavyofikia, kukusanya, kutumia na kushiriki data ya mtumiaji, lakini si tu data iliyofumbuliwa kwenye sehemu ya Usalama wa Data. Sharti ijumuishe:
Huluki (kwa mfano, msanidi programu, kampuni) iliyotajwa kwenye ukurasa wa programu katika Google Play inapaswa ionekane katika sera ya faragha au lazima jina la programu litajwe kwenye sera ya faragha. Programu zisizofikia data yoyote nyeti na ya binafsi ya mtumiaji zinapaswa pia kuwasilisha sera ya faragha. Tafadhali hakikisha kuwa sera yako ya faragha inapatikana kwenye URL inayotumika, inayoweza kufikiwa na umma na isiyo na mipaka pepe (hatukubali PDF). Masharti ya Kufuta AkauntiIkiwa programu yako huwaruhusu watumiaji kufungua akaunti kutoka ndani ya programu yako, basi ni lazima pia kuwaruhusu watumiaji kuomba akaunti zao zifufutwe. Watumiaji wanapaswa kuwa na chaguo linaloweza kutambulika kwa urahisi la kuanzisha ufutaji wa akaunti ya programu kutoka ndani na nje ya programu yako (k.m. kwa kutembelea tovuti yako). Kiungo cha nyenzo hii ya wavuti kinapaswa kuwekwa ndani ya sehemu ya fomu ya URL iliyobainishwa ndani ya Dashibodi ya Google Play. Unapofuta akaunti ya programu kutokana na ombi la mtumiaji, unapaswa pia kufuta data ya mtumiaji inayohusiana na akaunti hiyo ya programu. Kufunga akaunti kwa muda, kuzima au "kusimamisha" akaunti ya programu si sawa na kufuta akaunti. Ikiwa utahitaji kuhifadhi data fulani kwa sababu halali kama vile madhumuni ya usalama, kuzuia ulaghai au kutii mamlaka, unapaswa uwataarifu watumiaji wako kwa njia ya uwazi kuhusu taratibu zako za kuhifadhi data (kwa mfano, ndani ya sera yako ya faragha). Ili upate maelezo zaidi kuhusu masharti ya sera ya kufuta akaunti, tafadhali kagua makala haya ya Kituo cha Usaidizi. Kwa maelezo ya ziada kuhusu kusasisha fomu yako ya usalama wa data, tembelea makala haya. |
Matumizi ya Kitambulisho Kilichowekwa na ProgramuAndroid italeta kitambulisho kipya ili kusaidia katika matumizi ya hali muhimu kama vile takwimu na kuzuia ulaghai. Sheria na masharti ya vitambulisho hivi yapo hapo chini.
|
EU-U.S., Swiss Privacy Shield (Mifumo ya Faragha ya Uswizi, Marekani-Umoja wa Ulaya)Ukiwa unaweza kufikia, kutumia au kuchakata maelezo ya binafsi yaliyo kwenye Google na ambayo yanatambulisha mtu kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja na ikiwa maelezo hayo yametoka Umoja wa Ulaya au Uswizi ("Taarifa Binafsi kutoka Umoja wa Ulaya"), basi ni sharti:
Unapaswa kufuatilia jinsi unavyotii masharti haya kila wakati. Iwapo hutaweza kutimiza masharti haya wakati wowote ule (au iwapo kuna uwezekano mkubwa kuwa hutaweza kuyatimiza), unapaswa kutuarifu mara moja kwa kutuma barua pepe kwa data-protection-office@google.com na uache kuchakata Taarifa Binafsi za Umoja wa Ulaya mara moja au uchukue hatua zinazofaa za kurejesha kiwango cha ulinzi wa kutosha. Kuanzia tarehe 16 Julai 2020, Google haitegemei tena EU-U.S. Privacy Shield (Mfumo wa Faragha wa Ulaya-Marekani) ili kuhamisha data binafsi ambayo imetoka nchi washirika katika Makubaliano ya Kiuchumi ya Ulaya au Uingereza kwenda Marekani. (Pata maelezo zaidi.) Maelezo zaidi yanapatikana katika Kifungu cha tisa cha DDA. |