Mpango wa Sera

Sera zetu za Maudhui hutumika kwa maudhui yoyote yanayoonyeshwa au kuunganishwa na programu yako, ikiwa ni pamoja na matangazo yoyote inayoonyesha kwa watumiaji na maudhui yoyote yanayotokana na mtumiaji inayopangisha au kuunganisha. Zaidi ya hayo, yanatumika kwa maudhui yoyote kutoka kwa akaunti ya msanidi programu yanayoonyeshwa hadharani katika Google Play, ikiwa ni pamoja na jina lako la msanidi programu na ukurasa wa kutua wa tovuti yako ya msanidi programu iliyoorodheshwa.

Haturuhusu programu zinazowaruhusu watumiaji kusakinisha programu zingine kwenye vifaa vyao. Programu zinazotoa idhini ya kufikia programu zingine, michezo au programu zisizohitaji kusakinishwa, ikijumuisha vipengele na huduma zinazotolewa na washirika wengine, lazima zihahakikishe kwamba maudhui yote ambako zinatoa idhini ya kufikia yanatii Sera za Google Play na huenda pia yakapitia ukaguzi wa ziada wa sera.

Masharti yanayotumika katika sera hizi yana maana sawa na Mkataba wa Usambazaji kwa Wasanidi Programu (DDA). Mbali na kutii sera hizi na DDA, maudhui ya programu yako lazima yakadiriwe kulingana na Mwongozo wetu wa Ukadiriaji wa Maudhui.

Haturuhusu programu au maudhui ya programu ambayo yanadunisha imani ya watumiaji katika mfumo wa Google Play. Kwa kukagua iwapo tutajumuisha au kuondoa programu kutoka Google Play, tunazingatia vigezo kadhaa, ikiwa ni pamoja na, lakini si tu mtindo wa madhara au hatari kubwa na matumizi mabaya. Tunatambua hatari ya utumiaji mbaya ikiwa ni pamoja na, lakini si tu vipengee kama vile malalamiko yanayolenga programu na msanidi programu, kuripoti habari, historia ya ukiukaji wa awali, maoni ya watumiaji na matumizi ya chapa, herufi na vipengee vingine maarufu.

Jinsi Google Play Protect hufanya kazi

Google Play Protect hukagua programu unapozisakinisha. Pia hukagua kifaa chako mara kwa mara. Ikipata programu inayoweza kudhuru, inaweza:

  • Kukutumia arifa. Ili uondoe programu, gusa arifa, kisha uguse Ondoa.
  • kuzima programu hadi utakapoiondoa.
  • Kuondoa programu kiotomatiki. Katika hali nyingi, iwapo programu yenye madhara imetambuliwa, utapokea arifa itakayokuarifu kuwa programu iliondolewa.

Jinsi ya kutumia ulinzi dhidi ya programu hasidi

Ili kukulinda dhidi ya programu hatari za kampuni nyingine, URL na matatizo mengine ya usalama, Google inaweza kupokea maelezo kuhusu:

  • Muunganisho wa mtandao wa kifaa chako 
  • URL zinazoweza kuleta madhara 
  • Mfumo wa uendeshaji na programu zilizosakinishwa kwenye kifaa chako kupitia Google Play au vyanzo vingine.

Unaweza kupata onyo kutoka Google kuhusu programu au URL ambayo si salama. Programu au URL inaweza kuondolewa au kuzuiwa isisakinishwe na Google iwapo inatambuliwa kuwa hatari kwa vifaa, data au watumiaji.

Unaweza kuchagua kuzima baadhi ya vipengele hivi vya usalama kwenye mipangilio ya kifaa chako. Lakini Google inaweza kuendelea kupokea maelezo kuhusu programu zinazosakinishwa kupitia Google Play na programu zilizosakinishwa kwenye kifaa chako kutoka vyanzo vingine zinaweza kuendelea kukaguliwa ili kubaini matatizo ya usalama bila kutuma maelezo kwa Google.

Jinsi arifa za Faragha hufanya kazi

Google Play Protect itakuarifu programu ikiondolewa kwenye Duka la Google Play kwa sababu programu inaweza kufikia taarifa yako binafsi na utakua na chaguo la kuiondoa. 

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Menyu kuu
17440339781957598164
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
true
true
true
true
true
92637
false
false