Kudai Umiliki
Miongo kadhaa iliyopita, mashabiki walishiriki maonyesho au nyimbo wazipendazo kwenye kanda za mikusanyiko ya nyimbo. Leo hii, hali hiyo ya kushiriki na kutoa shukrani imehamishiwa mtandaoni. Maelfu ya studio za kurekodia muziki na wenye hakimiliki wana makubaliano ya leseni na YouTube ya kuchapisha video na kuchuma mapato kutokana nazo. Wanakubali kuwa ulimwengu ambapo mashabiki huonyesha upendo kwa wasanii wawapendao kwa kupakia video za tamasha na miseto ni jambo la kusherehekewa. Pia wanaona kwamba maudhui yaliyopakiwa na mashabiki yanaweza kuwa njia ya kuwashawishi watazamaji na kuboresha mauzo.
Yote haya yanawezekana kwa sababu Content ID huweka otomatiki mchakato wa kudhibiti haki. Shabiki anapopakia video kwenye YouTube, video hiyo hukaguliwa kwa kulinganishwa na hifadhidata ya maudhui yaliyotolewa na wamiliki wa maudhui. Inapopata maudhui yanayolingana, inaweka dai kwenye video hiyo kwa niaba ya mmiliki wa maudhui na kumwezesha kuamua anachotaka kifanyike kuhusiana na video hiyo. Asilimia 0.5 tu ya madai yote ya muziki ndiyo hutolewa na wahusika wenyewe; tunashughulikia asilimia 99.5 iliyosalia kwa usahihi wa asilimia 99.7. Leo hii, mapato yanayotokana na maudhui yaliyopakiwa na mashabiki huchangia asilimia 50 ya mapato ya sekta ya muziki kwenye YouTube.
Content ID imewezesha YouTube kulipa mabilioni ya dola kwenye sekta ya muziki na idadi hiyo inaongezeka pakubwa kila mwaka. Kwa hivyo inashangaza kuona baadhi ya studio za kurekodia muziki na wasanii wanaoashiria kuwa YouTube imeruhusu muziki mwingi “usio na leseni” kwenye mfumo wake na kuwazuia wasanii kuchuma mapato. Ukweli ni kwamba YouTube huchukulia mchakato wa kudhibiti hakimiliki kwa umakini sana na tunajitahidi kuhakikisha kuwa wenye hakimiliki wanachuma mapato bila kujali ni nani aliyepakia muziki wao. Hakuna mfumo mwingine unaotoa kiwango kikubwa hivyo cha mapato kwa watayarishi-- wakubwa na wadogo-- kwenye maudhui ya aina zote.
Kudhibiti Leseni za Muziki
Inahitaji seti nyingi tofauti za haki kucheza wimbo kwenye YouTube na kwa kawaida, kila mojawapo ya haki hizi hutolewa na mhusika tofauti. Kila mara wimbo unapotumiwa, malipo ya YouTube ni lazima yagawanywe miongoni mwa wenye hakimiliki hawa wengi kote ulimwenguni na kila mtu hupewa kiasi anachostahili.
Tunaamini kuwa uwazi ni muhimu katika kuhakikisha sekta ya muziki inawafaa wasanii, kwa hivyo hebu tuangalie haki na wenye hakimiliki ambao wanaweza kuhusika.
Haki za Matumizi ya Toleo Kuu
Haki za Utendaji wa Umma
Vipengee vyote vya muziki vilivyorekodiwa (rekodi kuu) vina kazi ya muziki ya msingi (utunzi) na seti tofauti za haki hutumika kwenye kazi hii ya msingi. Kwa madhumuni ya YouTube, haki hizi zinaweza kugawanywa katika aina mbili - haki za utendaji wa umma na haki nyingine.
Leseni za utendaji wa umma mara nyingi hudhibitiwa na mashirika ya haki za uonyeshaji (PRO). Mashirika ya Haki za Uonyeshaji (PRO) huhakikisha kuwa baa, mikahawa, sebule za hoteli, nk. zinalipia muziki unaotumika katika maeneo hayo. Wimbo unapotiririshwa kwenye YouTube, mashirika haya hukusanya mirabaha na kuisambaza kwa waandishi wa nyimbo na wachapishaji wa muziki ili kufidia utendaji wa umma wa utunzi husika. Mara nyingi, huluki ziitwazo “jamii za kukusanya mirabaha” zitawajibikia majukumu haya katika nchi nyingine. Mashirika haya yameteuliwa yashughulikie hatua za jumla za kudhibiti haki na mara kwa mara yatatoa leseni za jumla, ambazo zinamwezesha mwenye leseni kutumia katalogi nzima ya jamii ya kukusanya mirabaha kwa kipindi fulani, badala ya kupata leseni mahususi kwa kila kazi.