Programu za Simu Zisizotakikana

Mobile Unwanted Software

Hapa Google, tunaamini kuwa tukimzingatia mtumiaji, mengine yote yatatekelezwa. Katika Kanuni zetu za Programu na Sera ya Programu Isiyotakikana, tunatoa mapendekezo ya jumla kuhusu programu inayotoa hali bora ya utumiaji. Sera hii hutokana na Sera ya Google ya Programu Isiyotakikana kwa kubainisha kanuni za mfumo wa Android na Duka la Google Play. Programu inayokiuka kanuni hizi inaweza kuwa hatari kwa hali ya utumiaji na tutachukua hatua kulinda watumiaji dhidi yake.

Kama ilivyotajwa kwenye Sera ya Programu Isiyotakikana, tumegundua kuwa programu nyingi zisizotakikana huonyesha sifa moja au zaidi za msingi zinazofanana:

  • Ni ya kupotosha, inaahidi uboreshaji wa thamani ambao haiwezi kutekeleza.
  • Hujaribu kuwalaghai watumiaji kuisakinisha au hujificha katika programu nyingine ya kusakinishwa.
  • Haimfahamishi mtumiaji kuhusu kanuni na utendaji wake.
  • Huathiri mfumo wa mtumiaji kwa njia zisizotarajiwa.
  • Hukusanya au kutuma maelezo ya faragha bila kumfahamisha mtumiaji.
  • Hukusanya au kutuma maelezo ya faragha bila kushughulikiwa kiusalama (k.m. kutuma kupitia HTTPS)
  • Huunganishwa na programu nyingine na uwepo wake haufumbuliwi.

Kwenye vifaa vya mkononi, programu ni msimbo katika muundo wa programu, mfumo wa jozi, ubadilishaji wa mfumo, n.k. Ili kuzuia programu ambayo ni hatari kwa mfumo wa programu au inayokatiza hali ya utumiaji, tutachukua hatua kwa msimbo unaokiuka kanuni hizi.

Hapa chini, tunafafanua Sera ya Programu Isiyotakikana ili kubainisha utendaji wake kwenye programu ya simu. Sawa na ilivyo kwenye sera hiyo, tutaendelea kuboresha sera hii ya Programu Isiyotakikana ya Simu ili kushughulikia aina mpya za matukio ya matumizi mabaya.

Utendaji na ufumbuzi wazi

Misimbo yote inapaswa kutenda ilivyowaahidi watumiaji. Programu zinapaswa kutekeleza utendaji wote unaotajwa. Programu hazipaswi kuwachanganya watumiaji. 

  • Programu zinapaswa kuwa wazi kuhusu utendaji na malengo.
  • Kwa njia dhahiri na wazi, elezea mtumiaji mabadiliko kwenye mfumo yatakayosababishwa na programu. Waruhusu watumiaji kukagua na kuidhinisha chaguo na mabadiliko yote ya usakinishaji. 
  • Programu hazipaswi kuwakilisha kwa njia ya uongo hali ya kifaa cha mtumiaji, kwa mfano kudai kuwa mfumo uko katika hali hatari ya usalama au umeathiriwa na virusi.
  • Usitumie shughuli zisizo sahihi zilizobuniwa ili kuongeza watazamaji wa tangazo na/au walioshawishika.
  • Haturuhusu programu ambazo huwapotosha watumiaji kwa kuiga mtu mwingine (k.m. msanidi programu, kampuni, shirika jingine) au programu nyingine. Usidokeze kuwa programu yako inahusiana au imeidhinishwa na mtu, ilhali si kweli.

Mifano ya ukiukaji:

  • Ulaghai wa matangazo
  • Kuhadaa Watu

Kulinda data na faragha ya mtumiaji

Toa maelezo bayana kuhusu ufikiaji, matumizi, ukusanyaji na utumaji wa data nyeti na binafsi ya mtumiaji. Matumizi ya data ya mtumiaji ni lazima yatii sera zote husika za Data ya Mtumiaji, zinapotumika na yatilie maanani tahadhari zote za kulinda data hiyo.

  • Wape watumiaji fursa ya kukubali ukusanyaji wa data yao kabla ya kuanza kukusanya na kuituma kutoka kwenye kifaa, ikiwa ni pamoja na data kuhusu akaunti za wengine, barua pepe, namba ya simu, programu zilizowekwa kwenye vifaa, faili, data ya mahali na data nyingine yoyote nyeti na ya binafsi ambayo mtumiaji hatarajii ikusanywe.
  • Data nyeti na ya binafsi ya mtumiaji inayokusanywa inapaswa kushughulikiwa kwa njia salama, ikiwa ni pamoja na kutumwa kupitia usimbaji fiche wa kisasa (kwa mfano, kupitia HTTPS).
  • Ni lazima programu, ikiwa ni pamoja na programu za vifaa vya mkononi, zitume tu data nyeti na ya binafsi ya mtumiaji kwenye seva jinsi inavyohusiana na utendaji wa programu.
  • Usiwaombe au kuwadanganya watumiaji wazime vipengele vya ulinzi wa usalama wa kifaa kama vile Google Play Protect. Kwa mfano, hupaswi kutoa zawadi au vipengele vya ziada vya programu kwa watumiaji ili wazime Google Play Protect.

Mifano ya ukiukaji:

  • Ukusanyaji Data (linganisha Vidadisi)
  • Matumizi mabaya ya Ruhusa Zinazodhibitiwa

Mifano ya sera za Data ya Mtumiaji:

Usidhuru hali ya utumiaji wa vifaa vya mkononi 

Hali ya utumiaji inapaswa kuwa dhahiri, rahisi kueleweka na kulingana na chaguo zinazofanywa na mtumiaji. Inapaswa kuwasilisha kwa njia ya uwazi uboreshaji wa thamani kwa mtumiaji na isikatize hali ya utumiaji iliyotangazwa au inayopendelewa.

  • Usionyeshe matangazo yanayoonyeshwa kwa watumiaji kwa njia zisizotarajiwa, ikiwemo kuathiri au kuingilia urahisi wa kutumia vipengele vya kifaa, au kuonyesha nje ya mazingira ya programu bila kuweza kuondolewa kwa urahisi wala maelezo na idhini ya kutosha.
  • Programu hazipaswi kuingilia programu nyingine au kuathiri urahisi wa kutumia kifaa
  • Tukio la kuondoa programu, panapohitajika, linapaswa kuwa wazi. 
  • Programu ya kifaa cha mkononi haipaswi kuiga vidokezo kutoka mfumo wa uendeshaji wa kifaa au programu nyingine. Usizuie arifa za mtumiaji kutoka programu nyingine au mfumo wa uendeshaji, hasa zinazomfahamisha mtumiaji kuhusu mabadiliko katika mfumo wake wa uendeshaji. 

Mifano ya ukiukaji:

  • Matangazo yanayokatiza mtumiaji
  • Matumizi Yasiyoidhinishwa au Uigaji wa Mfumo wa Utendaji

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Menyu kuu
15620694603880563309
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
true
true
true
true
true
92637
false
false