Lengo letu kwa Programu za Android Zinazofunguka Papo Hapo ni kuunda mazingira bora na rahisi kwa watumiaji, na wakati huo huo kutii sera za usalama na faragha kwa kiwango cha juu. Sera zetu zimeundwa kutimiza lengo hilo.
Ni lazima wasanidi programu wanaochagua kusambaza Programu za Android zinazofunguka papo hapo kupitia Google Play watii sera zifuatazo, kando na Sera za Mpango wa Wasanidi Programu.
KitambulishoKwa programu zinazofunguka papo hapo zinazojumuisha kipengele cha maelezo ya kuingia katika akaunti, ni sharti wasanidi programu wajumuishe Smart Lock ya Manenosiri.
|
Uwezo wa Kutumia ViungoWasanidi wa Programu za Android Zinazofunguka Papo Hapo wanapaswa kutoa uwezo unaofaa wa kutumia viungo vya programu zingine. Iwapo programu za msanidi zinazofunguka papo hapo au zilizosakinishwa zina viungo ambavyo vinaweza kuelekeza kwenye programu inayofunguka papo hapo, ni lazima msanidi programu aelekeze watumiaji kwenye programu hiyo inayofunguka papo hapo badala ya, kwa mfano, kufungua viungo katika Mwonekano wa Wavuti.
|
Maelezo ya KiufundiNi lazima wasanidi programu watii masharti na maelezo ya kiufundi ya Programu za Android zinazofunguka papo hapo, yaliyotolewa na Google, kadri yanavyobadilishwa mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na zilizoorodheshwa kwenye hati yetu ya umma.
|
Kutoa Huduma ya Usakinishaji wa ProgramuProgramu inayofunguka papo hapo inaweza kumpa mtumiaji programu ambayo anaweza kusakinisha, lakini hili halipaswi kuwa lengo kuu la programu inayofunguka papo hapo. Wasanidi programu wanapotoa huduma ya usakinishaji:
Maelezo ya ziada ya programu inayofunguka papo hapo na mwongozo wa UX yanaweza kupatikana kwenye Mbinu Bora za Hali ya Utumiaji. |
Trafiki ya mtandaoTrafiki ya mtandao kutoka ndani ya programu inayofunguka papo hapo inapaswa kusimbwa kwa njia fiche kwa kutumia itifaki ya TLS kama vile HTTPS.
|