Programu za Android Zinazofunguka Papo Hapo

Lengo letu kwa Programu za Android Zinazofunguka Papo Hapo ni kuunda mazingira bora na rahisi kwa watumiaji, na wakati huo huo kutii sera za usalama na faragha kwa kiwango cha juu. Sera zetu zimeundwa kutimiza lengo hilo.

Ni lazima wasanidi programu wanaochagua kusambaza Programu za Android zinazofunguka papo hapo kupitia Google Play watii sera zifuatazo, kando na Sera za Mpango wa Wasanidi Programu.

 

Kitambulisho

Kwa programu zinazofunguka papo hapo zinazojumuisha kipengele cha maelezo ya kuingia katika akaunti, ni sharti wasanidi programu wajumuishe Smart Lock ya Manenosiri.

 

Uwezo wa Kutumia Viungo

Wasanidi wa Programu za Android Zinazofunguka Papo Hapo wanapaswa kutoa uwezo unaofaa wa kutumia viungo vya programu zingine. Iwapo programu za msanidi zinazofunguka papo hapo au zilizosakinishwa zina viungo ambavyo vinaweza kuelekeza kwenye programu inayofunguka papo hapo, ni lazima msanidi programu aelekeze watumiaji kwenye programu hiyo inayofunguka papo hapo badala ya, kwa mfano, kufungua viungo katika Mwonekano wa Wavuti.

 

Maelezo ya Kiufundi

Ni lazima wasanidi programu watii masharti na maelezo ya kiufundi ya Programu za Android zinazofunguka papo hapo, yaliyotolewa na Google, kadri yanavyobadilishwa mara kwa mara, ikiwa ni pamoja na zilizoorodheshwa kwenye hati yetu ya umma.

 

Kutoa Huduma ya Usakinishaji wa Programu

Programu inayofunguka papo hapo inaweza kumpa mtumiaji programu ambayo anaweza kusakinisha, lakini hili halipaswi kuwa lengo kuu la programu inayofunguka papo hapo. Wasanidi programu wanapotoa huduma ya usakinishaji:

  • Wanapaswa kutumia aikoni ya Usanifu Bora ya "pakua programu" na lebo ya "sakinisha" katika kitufe cha kusakinisha.
  • Hawapaswi kuwa na zaidi ya vidokezo 2-3 vya usakinishaji katika programu yao inayofunguka papo hapo.
  • Hawapaswi kutumia bango au mbinu nyingine inayofanana na matangazo kuwasilisha kidokezo cha usakinishaji kwa watumiaji.

Maelezo ya ziada ya programu inayofunguka papo hapo na mwongozo wa UX yanaweza kupatikana kwenye Mbinu Bora za Hali ya Utumiaji.

 

Kubadilisha Hali ya Kifaa

Programu zinazofunguka papo hapo hazipaswi kufanya mabadiliko kwenye kifaa cha mtumiaji ambayo yatadumu kwa zaidi ya kipindi ambacho programu inayofunguka papo hapo itatumika. Kwa mfano, programu zinazofunguka papo hapo hazipaswi kubadilisha mandhari ya mtumiaji au kuunda wijeti za skrini ya kwanza.

 

Kuonekana kwa Programu

Ni lazima wasanidi programu wahakikishe kwamba programu zinazofunguka papo hapo zinaonekana kwa mtumiaji, ili kwamba mtumiaji aweze kujua kila wakati programu inayofunguka papo hapo inapotumika kwenye kifaa chake.

 

Vitambulishi vya Vifaa

Programu zinazofunguka papo hapo haziruhusiwi kufikia vitambulishi vya vifaa ambavyo (1) vitaendelea kutumika baada ya programu inayofunguka papo hapo kufungwa na (2) mtumiaji hawezi kubadilisha mipangilio yake. Kwa mfano:

  • Nambari ya Muundo
  • Anwani za Mac za chipu zozote za mtandao
  • IMEI, IMSI

Programu zinazofunguka papo hapo zinaweza kufikia nambari za simu ikiwa zilipatikana kupitia ruhusa za muda ambao programu inatumika. Msanidi programu hapaswi kujaribu kukusanya maelezo ya vitambulishi hivi au mbinu nyingine ile kwa kusudi la kumtambua mtumiaji.

 

Trafiki ya mtandao

Trafiki ya mtandao kutoka ndani ya programu inayofunguka papo hapo inapaswa kusimbwa kwa njia fiche kwa kutumia itifaki ya TLS kama vile HTTPS.

 

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Menyu kuu
5215065520077591457
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
true
true
true
true
true
92637
false
false