Sera yetu ya programu hasidi ni rahisi. Inabaini kuwa mfumo wa Android, ikiwa ni pamoja na Duka la Google Play na vifaa vya watumiaji, havifai kuwa na shughuli za kihasidi (yaani programu hasidi). Kupitia kanuni hii kuu, tunajitahidi kutoa mfumo salama wa Android kwa watumiaji wetu na vifaa vyao vya Android.
Programu hasidi ni msimbo wowote unaoweza kuhatarisha mtumiaji, data ya mtumiaji au kifaa. Programu hasidi ni pamoja na Programu Zinazoweza Kudhuru (PHA), mfumo wa jozi au ubadilishaji wa mifumo, zikiwemo aina kama vile programu za Trojan, za wizi wa data binafsi na za vidadisi na tunaendelea kusasisha na kuweka aina mpya.
Ingawa programu hasidi hutofautiana katika uwezo na aina, kwa kawaida zina mojawapo ya malengo yafuatayo:
- Kuhatarisha ukamilifu wa kifaa cha mtumiaji.
- Kupata udhibiti wa kifaa cha mtumiaji.
- Kuruhusu utendaji unaodhibitiwa kwa mbali ili mshambulizi aweze kufikia, kutumia au kukagua kifaa kilichoathiriwa.
- Kusambaza data ya binafsi au kitambulisho kutoka kwenye kifaa bila ufumbuzi na idhini inayofaa.
- Kusambaza taka au amri kutoka kwenye kifaa kilichoathiriwa ili kuathiri mitandao na vifaa vingine.
- Kulaghai watumiaji.
Programu, mfumo wa jozi au ubadilishaji wa mfumo unaweza kuwa hatari, kwa hivyo unaweza kusababisha shughuli za kihasidi, hata kama haukukusudiwa kuwa hatari. Hii ni kwa sababu programu, mifumo ya jozi au ubadilishaji wa mfumo unaweza kufanya kazi kwa namna tofauti kulingana na vipengee mbalimbali. Kwa hivyo, kitu ambacho ni hatari kwa kifaa kimoja cha Android huenda kisihatarishe kifaa kingine cha Android. Kwa mfano, kifaa kinachotumia toleo jipya la Android hakiathiriwi na programu hatari zinazotumia API zilizoacha kutumika katika kutekeleza shughuli za kihasidi lakini kifaa ambacho bado kinatumia toleo la awali zaidi la Android kinaweza kuwa hatarini. Programu, mfumo wa jozi au ubadilishaji wa mfumo huripotiwa kuwa programu hasidi au PHA iwapo inahatarisha kwa uwazi vifaa na watumiaji wote wa Android au baadhi yao.
Aina za programu hasidi zilizo hapa chini, zinaonyesha imani yetu ya msingi kwamba ni sharti watumiaji waelewe jinsi vifaa vyao vinavyotumiwa na wadumishe mfumo salama unaoruhusu uvumbuzi imara na hali ya utumiaji inayoaminika.
Tembelea Google Play Protect ili upate maelezo zaidi.
KUNJA ZOTE PANUA ZOTE
Programu za kudadisiMsimbo unaokusanya data nyeti au binafsi ya mtumiaji kutoka kwenye kifaa kisha kutuma data hiyo kwa mshirika mwingine (biashara au mtu mwingine) kwa madhumuni ya ufuatiliaji. Ni lazima programu zitoe ufumbuzi dhahiri wa kutosha na zipate idhini kama inavyotakiwa kwa mujibu wa Sera ya Data ya Mtumiaji. Mwongozo kwa ajili ya Programu za Ufuatiliaji Programu ambazo zimebuniwa na kutangazwa mahususi kwa ajili ya kufuatilia mtu mwingine, kwa mfano wazazi kufuatilia watoto wao au udhibiti wa kibiashara kwa ajili ya ufuatiliaji wa wafanyakazi, ndiyo programu pekee za ufuatiliaji zitakazokubalika, ilimradi programu hizo zinatii masharti yaliyofafanuliwa hapa chini. Programu hizi hazipaswi kutumiwa kufuatilia mtu yeyote mwingine (kwa mfano, mume au mke) hata kama akijua na kukuruhusu, bila kujali iwapo arifa ya kudumu inaonyeshwa. Ni lazima programu hizi zitumie kitia alama cha metadata cha IsMonitoringTool kwenye faili ya maelezo ili ziweze kujibainisha inavyofaa kuwa programu za ufuatiliaji. Programu za ufuatiliaji zinapaswa kutii masharti yafuatayo:
Tafadhali rejelea makala ya Matumizi ya Kitia alama cha isMonitoringTool ya Kituo cha Usaidizi ili upate maelezo zaidi. |
TakaMsimbo unaotuma ujumbe ambao mtumiaji hajaomba atumiwe kwenye anwani yake au unaotumia kifaa kutuma barua taka.
|
VidadisiVidadisi ni mienendo, misimbo au programu hasidi zinazokusanya, kuondoa au kutuma data ya mtumiaji au ya kifaa isiyohusiana na utendaji wa kutii sera. Mienendo au misimbo hasidi inayoweza kuzingatiwa kuwa ya kumdadisi mtumiaji au kuondoa data bila ilani au idhini inayofaa pia huchukuliwa kuwa vidadisi. Kwa mfano, ukiukaji wa vidadisi ni pamoja na, lakini si tu:
Ni lazima programu zote zitii Sera zote za Mpango wa Wasanidi Programu wa Google Play, ikiwa ni pamoja na sera za data ya mtumiaji na ya kifaa kama vile Programu za Simu Zisizotakikana, Data ya Mtumiaji, Ruhusa na API Zinazofikia Taarifa Nyeti na Masharti ya SDK. |