Masharti ya kiwango lengwa cha API kwa programu za Google Play

Ili kuweka wazi zaidi makataa ya Kiwango Lengwa cha API, tunaunganisha tarehe hadi tarehe 31 Agosti kila mwaka.

Kuanzia tarehe 31 Agosti 2023:

  • Ni sharti programu mpya zilenge Android 13 (Kiwango cha API cha 33) au mpya zaidi; isipokuwa kwa programu za Wear OS, ambazo lazima zilenge Android 11 (Kiwango cha API cha 30) au hadi Android 13 (Kiwango cha API cha 33).
  • Ni sharti programu zilizopo zilenge kiwango cha API cha 31 au mpya zaidi ili ziendelee kupatikana kwenye vifaa vya watumiaji vinavyotumia mfumo wa uendeshaji wa Android ulio juu zaidi ya kiwango lengwa cha API cha programu yako. Programu zinazolenga kiwango lengwa cha API cha 30 au chini yake (kiwango lengwa cha API cha 29 au chini yake kwa Wear OS), zitapatikana tu kwenye vifaa vinavyotumia mfumo wa uendeshaji wa Android ulio sawa au chini ya kiwango lengwa cha API cha programu yako.
Utaweza pia kuomba uongezewe muda hadi tarehe 1 Novemba 2023, ikiwa unahitaji muda zaidi wa kusasisha programu yako. Utaweza kufikia fomu za kuomba kuongezewa muda wa programu yako katika Dashibodi ya Google Play mwanzoni mwa mwezi wa Agosti ikiwa umeathirika, kupitia ukurasa wa Hali ya sera kwa kubofya hadi kwenye onyo au hitilafu husika.

Kila toleo jipya la Android huleta mabadiliko yanayoboresha hali ya utumiaji, usalama na utendaji wa mfumo wa Android kwa ujumla. Kila programu hubainisha targetSdkVersion (pia hujulikana kama kiwango lengwa cha API) katika faili ya maelezo. Kiwango lengwa cha API huashiria jinsi programu yako inavyotakiwa kufanya kazi kwenye matoleo tofauti ya Android.

Hali ya kuweka mipangilio kwenye programu yako ili ilenge kiwango cha API ya hivi karibuni huhakikisha kwamba watumiaji wananufaika kutokana na maboresho ya usalama, faragha na utendaji, huku ikiruhusu programu itumike kwenye matoleo ya awali ya Android (hadi toleo la minSdkVersion lililobainishwa).

Ili kuwapa watumiaji wa Android na Google Play utumiaji salama, Google Play inahitaji programu zote zitimize masharti ya kiwango lengwa cha API yaliyoorodheshwa hapa chini.

Hali zisizofuata masharti haya zinajumuisha:

  • Programu binafsi zinazotumiwa tu na watumiaji katika shirika mahususi na zinalenga tu usambazaji wa ndani ya shirika. 
  • Programu za Android Automotive OS zilizojumuishwa ndani ya kifurushi kimoja zitaendelea kupatikana kwa watumiaji wote wa Google Play.

Ufafanuzi

Programu mpya Programu ambayo bado haijachapishwa katika Google Play (kwa mfano, programu mpya kabisa).
Programu iliyopo Programu ambayo imechapishwa kwenye Google Play.
Sasisho la programu Toleo jipya la programu ambalo unawasilisha kwa ajili ya ukaguzi ili lichukue nafasi ya programu iliyopo.

Masharti ya sasisho la programu

Toleo la mfumo wa uendeshaji wa Android
(Kiwango cha API)

Je, programu mpya na masasisho ya programu mpya yatahitajika kulenga kiwango hiki cha API lini?
Programu mpya Masasisho ya programu

Android 13 (kiwango cha API cha 33)*

Tarehe 31 Agosti, 2023

Tarehe 31 Agosti, 2023

Android 12 (kiwango cha API cha 31)

Tarehe 31 Agosti, 2022

Tarehe 1 Novemba, 2022

*Ili kusaidia kurahisisha mabadiliko kwa wasanidi programu, wasanidi programu wataweza kuomba muda zaidi hadi tarehe 1 Novemba.

Kidokezo: Ili upate mwongozo wa kiufundi kuhusu jinsi ya kubadilisha kiwango cha API kinacholengwa na programu yako ili kutimiza masharti haya, rejelea mwongozo wa uhamishaji.

Masharti ya programu ya Wear OS

Toleo la mfumo wa uendeshaji wa Android (Kiwango cha API)

Je, ni wakati gani mawasilisho ya programu ya Wear OS yanahitajika kulenga Kiwango hiki cha API?
Programu mpya Masasisho ya programu
Android 11 (Kiwango cha API cha 30) (hamna mabadiliko) Tarehe 1 Agosti, 2022 Tarehe 1 Novemba, 2022

Masharti ya upatikanaji wa programu

Kwa sasa, programu zilizopo (kwenye vifaa vya mkononi, Android Auto, Android TV) lazima zilenge kiwango cha API cha 31 au mpya zaidi kufikia tarehe 31 Agosti 2023 (kiwango lengwa cha API cha 30 au mpya zaidi na kiwango lengwa cha 33 kwa Wear OS). Vinginevyo zitaacha kugundulika kwa watumiaji wote wa Google Play ambao vifaa vyao vinatumia matoleo ya mfumo wa uendeshaji wa Android ambayo ni mapya kuliko kiwango cha API kinacholengwa na programu yako, kwa sababu programu yako haikuundwa ili kukidhi viwango vya usalama na ubora ambavyo watumiaji hawa wanavitarajia kutoka kwenye matoleo mapya zaidi ya mfumo wa uendeshaji wa Android.

  • Programu zenye kiwango lengwa cha Android 11 (Kiwango cha API cha 30)* au chini yake hazitapatikana kwa watumiaji wapya wanaotumia mfumo wa uendeshaji wa Android wa juu zaidi kuliko kiwango lengwa cha API cha programu baada ya tarehe 31 Agosti 2023.
  • Programu zenye kiwango lengwa cha Android 10 (Kiwango cha API cha 29) au chini yake hazitapatikana kwa watumiaji wapya wanaotumia mfumo wa uendeshaji wa Android wa juu zaidi kuliko kiwango lengwa cha API cha programu baada ya tarehe 1 Novemba 2022 au tarehe 1 Mei 2023, iwapo programu yako iliongezewa muda.

*Ili kusaidia kurahisisha mabadiliko kwa wasanidi programu, wasanidi programu wataweza kuomba muda zaidi hadi tarehe 1 Novemba 2023. Utaweza kufikia fomu za kuomba kuongezewa muda za programu yako katika Dashibodi ya Google Play mwanzoni mwa mwezi wa Agosti iwapo umeathirika, kupitia ukurasa wa Hali ya sera kwa kubofya hadi kwenye hitilafu husika.


Hatua za kuchukua ili utii

Programu mpya

Programu zilizopo

Unapochapisha programu mpya, ni lazima ulenge API ya 33 au zaidi.

Ikiwa kiwango lengwa cha API cha programu yako iliyopo ni 31 au zaidi, basi programu yako inatii sera hii.

Ikiwa ulengaji wa programu yako iliyopo upo chini ya API ya 31, programu itaacha kupatikana kwa watumiaji wote wa Google Play ambao vifaa vyao vinatumia matoleo ya mfumo wa uendeshaji wa Android ambayo ni mapya kuliko kiwango cha API kinacholengwa na programu zako, kwa sababu programu yako haikuundwa ili kukidhi viwango vya usalama na ubora ambavyo watumiaji hawa wanavitarajia kutoka kwenye matoleo mapya zaidi ya mfumo wa uendeshaji wa Android.

  • Ikiwa unapanga kusasisha programu hii iwe katika kiwango lengwa kipya zaidi cha API, unaweza kutuma ombi la kuongezewa muda ili uendelee kusambazwa kwa watumiaji wote kwenye Google Play hadi tarehe 1 Novemba 2023. Programu zilizoathirika zitapokea maonyo ya sera na ujumbe katika kikasha kwenye Dashibodi ya Google Play, na utaweza kufikia fomu ya maombi ukiwa ndani ya ukurasa wa maelezo wa onyo au hitilafu, inayofikiwa kupitia ukurasa wa Hali ya sera.
Unaposasisha programu yako, ni lazima ulenge API ya 33 au zaidi.


Masharti ya Wear OS

Programu mpya

Programu zilizopo

Unapochapisha programu mpya, ni sharti ulenge API ya 30 au mpya zaidi hadi Android 13 (Kiwango cha API cha 33).

Ikiwa kiwango lengwa cha API cha programu yako iliyopo ni 30 au mpya zaidi hadi Android 13 (Kiwango cha API 33), basi programu yako inatii sera hii.

Ikiwa ulengaji wa programu yako iliyopo upo chini ya API ya 30, programu itaacha kupatikana kwa watumiaji wote wa Google Play ambao vifaa vyao vinatumia matoleo ya mfumo wa uendeshaji wa Android ambayo ni mapya kuliko kiwango cha API kinacholengwa na programu zako, kwa sababu programu yako haikuundwa ili kukidhi viwango vya usalama na ubora ambavyo watumiaji hawa wanavitarajia kutoka kwenye matoleo mapya zaidi ya mfumo wa uendeshaji wa Android.

  • Ikiwa unapanga kusasisha programu hii iwe katika kiwango lengwa cha API cha 30, unaweza kutuma ombi la kuongezewa muda ili uendelee kusambaza kwa watumiaji wote kwenye Google Play hadi tarehe 1 Novemba 2023. Programu zilizoathirika zitapokea maonyo ya sera na ujumbe katika kikasha kwenye Dashibodi ya Google Play, na utaweza kufikia fomu ya maombi ukiwa ndani ya ukurasa wa maelezo wa onyo au hitilafu, inayofikiwa kupitia ukurasa wa Hali ya sera.
Unaposasisha programu yako, ni sharti ulenge API ya 30 au hadi Android 13 (Kiwango cha API cha 33).

Maswali yanayoulizwa sana

Kwa programu zinazolenga API ya 30 au ya chini zaidi

Nina programu iliyochapishwa kwenye Google Play ambayo inalenga API ya 30 au ya chini zaidi (kwa Wear OS, programu inayolenga API ya 29 au chini zaidi), ambayo sina mpango wa kuisasisha. Je, nina chaguo gani?

Ikiwa ungependa programu hii iendelee kutumika kwa watumiaji wako waliopo, huhitaji kufanya kitu chochote. Hata hivyo, programu yako haitapatikana katika Google Play kwa watumiaji wapya wanaotumia vifaa vyenye mfumo wa uendeshaji wa Android mpya zaidi ya kiwango lengwa cha programu yako. Itapatikana tu kwa watumiaji wa Google Play wanaotumia vifaa vyenye mfumo wa uendeshaji wa Android wenye Kiwango cha API cha programu yako au chini zaidi.

Kufikia tarehe 1 Agosti, 2023, ni lazima programu yako itimize masharti ya kiwango hiki lengwa cha API, vinginevyo itasitisha kutambulika kwa watumiaji wote wa Google Play ambao vifaa vyao vinatumia matoleo mapya zaidi ya mfumo wa uendeshaji wa Android kuliko kiwango lengwa cha API cha programu yako.

Ikiwa unapanga kusasisha programu yako iwe katika kiwango lengwa kipya zaidi cha API na unahitaji muda zaidi baada ya tarehe 31 Agosti, unaweza kuomba uongezewe muda ili uendelee kusambaza kwa watumiaji wote wa Google Play hadi tarehe 1 Novemba. Fomu ya kuomba kuongezewa muda itapatikana baadaye mwaka huu katika Dashibodi ya Google Play.

Ikiwa ungependa kusitisha matumizi ya programu yako kwa watumiaji wapya hata kwenye vifaa vya zamani, unaweza kubatilisha uchapishaji wa programu yako.

Je, nitapata wapi fomu ya kuongezewa muda ili kuendelea kusambaza programu kwa watumiaji wa Google Play hadi tarehe 1 Novemba, 2023?

Programu tu ambazo hazitii sera hii ndizo zitapokea maonyo ya sera na ujumbe unaotumwa kwenye Kikasha cha Dashibodi ya Google Play. Fomu ya kuomba kuongezewa muda inapatikana kupitia ukurasa wa maelezo wa onyo au hitilafu, inayopatikana kwenye ukurasa wa Hali ya sera ya Dashibodi ya Google Play.

Nina programu ambazo sitaki tena zichapishwe kwenye Google Play. Ninaweza kufanya nini?

Kwa maelekezo ya jinsi ya kubatilisha uchapishaji wa programu yako, angalia Sasisha au batilisha uchapishaji wa programu yako.

Je, watumiaji wangu ambao walishapakua programu yangu awali wataathiriwa vipi?

Watumiaji ambao walisakinisha programu hapo awali kutoka Google Play hawataathiriwa na bado watakuwa na uwezo wa kugundua, kusakinisha upya na kutumia programu kwenye toleo lolote la mfumo wa uendeshaji wa Android ambao programu yako itakubali.

Je, sasisho hili litaathiri upakuaji wa programu?

Huenda likaathiri viwango vya upakuaji wa programu yako iwapo watumiaji wapya wenye vifaa vilivyo na matoleo mapya zaidi ya mfumo wa uendeshaji wa Android watashindwa kugundua au kupakua programu yako kutoka kwenye Google Play.

Je, hali ya utumiaji itakuwaje ikiwa mtumiaji mwenye kifaa kipya zaidi atatembelea kiungo mahususi cha ukurasa wa duka la programu, lakini programu inalenga API ya 30 au ya chini zaidi?

Google Play itamtaarifu mtumiaji kuwa "programu hii haiwezi kusakinishwa kwenye kifaa chake kwa sababu ilitengenezwa kwa ajili ya toleo la zamani la Android."

Je, kuna hali zozote zisizofuata kanuni kwa programu zilizopo zinazolenga API ya 30 au ya chini zaidi?

Ndiyo. Hatujumuishi programu ambazo ni za faragha kabisa zinazotumiwa tu na watumiaji katika shirika mahususi na zinalenga tu usambazaji wa ndani ya shirika na programu zinazolenga umbo la Android Automotive OS.

Je, maelezo haya yamekufaa?

Tunawezaje kuboresha?

Je, unahitaji usaidizi mwingine?

Jaribu hatua zifuatazo:

Tafuta
Futa utafutaji
Funga kisanduku cha kutafutia
Menyu kuu
6472884614881634878
true
Tafuta kwenye Kituo cha Usaidizi
true
true
true
true
true
92637
false
false